Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Wednesday, December 26, 2012

SIMBA: MKUTANO WA DESEMBA 30 NI BATILI

Msemaji wa Simba Ezekiel Kamwaga.
26/12/2012
 TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
KHERI ya Krismas na Mwaka mpya kwenu nyote.
Uongozi wa klabu ya Simba leo unapenda kutoa taarifa ifuatayo kwenu.
  1. Mkutano wa Wanachama uliopangwa kufanyika Desemba 30 mwaka huu.
UONGOZI umepata taarifa kuwa kuna kundi la wanalojiita wanachama wa Simba waliopanga kufanya mkutano wa wanachama siku ya tarehe 30 Desemba mwaka huu (Jumapili hii) kwa lengo la kujadili mambo ya klabu.
Mkutano huo, kwa mujibu wa Katiba ya Simba ni batili. Ubatili huo unatokana na ukweli kwamba wale walioutisha mkutano huo hawana Locus Standi (nguvu au mamlaka) ya kufanya hivyo. Katiba ya Simba iko wazi kuwa mtu anayeitisha mkutano wa wanachama ni MWENYEKITI wa klabu pekee na si vinginevyo.
Mkutano huo wa wanachama haujaitishwa na Mwenyekiti wa klabu na hivyo hauna uhalali wowote wa kisheria.
Uchunguzi uliofanywa na klabu umebaini kwamba zaidi ya nusu ya walioitisha mkutano huo pia si wanachama halali wa Simba. Wengine hawajawahi kulipa ada zao za uanachama katika kipindi cha hadi miaka 10 iliyopita !
Matendo yanayofanywa na kundi hili yanaashiria watu wanaotaka tu kuleta vurugu klabuni. Kundi hili linafanya hivi wakati Rais Jakaya Kikwete ametoka kutoa kauli kuhusiana na namna vurugu zinavyosababisha kushuka kwa michezo hapa nchini.
Kundi hili linaandaa vurugu katika kipindi ambacho uongozi upo katika mikakati kabambe ya kuiboresha timu ikiwamo kuipeleka nje ya nchi kufanya mazoezi, jambo ambalo halijawahi kufanyika katika kipindi cha miaka 20 iliyopita.
Linaandaa vurugu katika kipindi ambacho Simba ndiyo bingwa mtetezi wa Ligi Kuu ya Tanzania na ikiwa imeongoza ligi katika msimu huu kuanzia mechi ya kwanza hadi ya 11 katika mechi 13 za kwanza.
Klabu inaomba wapenzi na wanachama wake kukaa mbali na kundi hili la waleta vurugu. Huu ni wakati ambapo tunatakiwa kuwa pamoja kwa vile klabu inatakiwa kutetea ubingwa wake na pia kuliwakilisha taifa katika michuano ya kimataifa mapema mwakani.
Huu ni wakati wa wanachama, wapenzi na uongozi kuwa kitu kimoja. Uongozi uko tayari kukosolewa wakati wowote ule lakini haukubaliani na waleta vurugu.
Uongozi unapenda kusisitiza lifuatalo, Mkutano wa Desemba 30 ni batili na wale wote wenye mapenzi mema na klabu wanatakiwa kukaa mbali nao na kutojihusisha kwa chochote na wanaopanga vurugu.
Imetolewa na
Ezekiel Kamwaga
Ofisa Habari
Simba SC

No comments:

Post a Comment