Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Thursday, December 20, 2012

SALUM KINJE WA SIMBA MGONJWA, ASHINDWA KUFANYA MAZOEZI

KIUNGO wa Simba Salim Kinje leo alishindwa kufanya mazoezi ya asubuhi na wenzake kutokana na kuugua malaria

Simba ambao ni mabingwa watetezi wa ligi kuu wanafanya mazoezi ya ufukweni  Coco Beach jijini Dar es Salaam wakijiandaa na mzunguko wa pili.

Akizungumza nleo jijini wakati wenzake wakiwa mazoezini Kinje alisema kuwa ugonjwa huo ulimuanza tangu juzi na kwamba anaendelea kutumia dawa.

"Sijajumuika na wenzangu kwani naumwa na malaria ambayo yalinianza jana(juzi) lakini hata hivyo naendelea vizuri kwani dawa ninazotumia zinanisaidia," alisema.

Wakati huo huo wachezaji wa kikosi hicho wamefurahishwa kumuona kiungo mchezeshaji Haruna Moshi 'Boban' akijumuika nao katika mazoezi hayo.

Ramadhani Chombo 'Redondo' alisema kuwa Haruna Moshi ni mchezaji muhimu sana na kwamba kikosi chao kitazidi kuimarika.

"Sisi hatuna kubwa la kuongea zaidi ya kufurahi kumuona akijumuika nasi katika mazoezi,hii inaashiria kuwa timu inazidi kuimarika," alisema.

Mara baada ya mazoezi hayo kumalizika majira ya saa 2:56 asubuhi Boban alipanda gari yake aina ya Toyota Corola yenye namba za usajili T4920 CAT na kuondoka.

Boban alisimamishwa na uongozi wa timu hiyo baada ya kudanganya kuwa ni mgonjwa na kuachwa katika safari ya kwenda Tanga kupambana na Mgambo Shooting.

Hata hivyo kesho yake wakati Simba ikikwaana na Mgambo katika uwanja wa Mkwakwani Boban alionekana jijini Dar es Salaam akicheza mpira wa mchangani maarufu kama 'Ndondo'.

No comments:

Post a Comment