Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, September 29, 2012

HYPER FC NA ANTA SHOBO FAINALI KESHO CHANIKA

Mchezaji wa Italian FC ya Chanika akikimbia na mpira huku mchezaji wa Hyper FC ya Gongolamboto wakati wa mchezo wa nusu fainali ambapo Italian walifungwa bao 1-0
TIMU za Hyper FC na Anta Shobo FC zote za Gongolamboto leo zitapambana kutafuta bingwa wa mashindano ya Beila.

Fainali hizi za vijana wa U-14 zitachezwa uwanja wa Chanika uliopo nje ya manispaa ya Ilala kuanzia saa 10.00 jioni na zinatarajiwa kuhudhuriwa na mashabiki wengi.

Timu ya Hyper Fc iliingia fainali baada ya kuifunga Italian Fc ya Chanika bao 1-0 kwenye mchezo wa nusu fainali uliochezwa uwanja huo wa Chanika na kuhudhuriwa na watazamaji wengi.

Nayo Anta Shobo wao waliifunga Kipawa Fc 4-1 na kufanikiwa kutinga fainali

Akizungumza na HABARI ZA MICHEZO, Mratibu wa Mashindano Abdallah Kinyogoli alisema mashindano yalianza kutimua vumbi Septemba mosi mwaka huu na jumla timu 8 za vijana wa umri wa chini ya miaka 14 zilishiriki.

"Mashindano yalikuwa mazuri na nashukuru lengo la kuibua na kuendeleza vipaji limefanikiwa na nategemea kuanzisha mashindano mengine ili kuwapa fursa wachezaji chipukizi kucheza michezo mingi ili wapate uzoefu" alisema Abdallah.

Bingwa atapata zawadi ya Mbuzi mwenye thamani ya 60,000 na mshindi wa pili atapata mpira mmoja

No comments:

Post a Comment