Akitwaa Tuzo hii, Ronaldo, anaechezea Real Madrid na Nchi yake Portugal, aliwashinda kwa Kura Lionel Messi na Antoine Griezmann.
Ronaldo pia alitwaa, mapema Mwezi Desemba, Tuzo ya Mchezaji Bora Duniani kwa 2016, Ballon d’Or, inayotolewa na Jarida la France, France Football, Tuzo ambayo kabla ya hapo, kwa Miaka 6, iliunganishwa na FIFA na kuitwa FIFA Ballon d’Or, lakini kuanzia safari hii wametengana.
Kocha Bora Duniani kwa Wanaume ni Claudio Ranieri baada ya kuiwezesha Leicester City, bila kutegemewa, kutwaa Ubingwa wa England kwa mara ya kwanza katika Historia yao.
MCHEZAJI BORA WANAUME:
-Wagombea: Cristiano Ronaldo, Antoine Griezmann, Lionel Messi
-Mshindi: Cristiano Ronaldo
MCHEZAJI BORA WANAWAKE:
-Wagombea: Melanie Behringer, Carli Lloyd, Marta
-Mshindi: Carli Lloyd wa USA.

-Wagombea: Claudio Ranieri, Fernando Santos, Zinedine Zidane
-Mshindi: Claudio Ranieri wa Mabingwa wa England Leicester City
KOCHA BORA WANAWAKE:
-Wagombea: Jill Ellis, Silvia Neid, Pia Sundhage
-Mshindi: Silvia Neid [Germany]
GOLI BORA [Tuzo ya Puskas]:
-Wagombea: Marlone, Daniuska Rodriguez, Mohd Faiz Subri
-Mshindi: Mohd Faiz Subri wa Penang, Malaysia.
Tuzo hii inatokana na Kura za Mashabiki Duniani kote.
TUZO TOKA KWA MASHABIKI:
-Wagombea: Mashabiki wa Den Haag, Borussia Dortmund & Liverpool na Iceland.
-Mshindi: Mashabiki wa Borussia Dortmund & Liverpool
TUZO YA UCHEZAJI WA HAKI
-Mshindi: Atletico Nacional ya Colombia
FIFA FIFPro World11 2016 – Kikosi Bora cha Mwaka 2016:
-Kipa: Neur
-Mabeki: Alves, Pique, Ramos, Marcelo
-Viungo: Modric, Kroos, Iniesta
-Mafowadi: Suarez, Ronaldo, Messi
No comments:
Post a Comment