Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Tuesday, March 10, 2015

CHRIS BRUNT AFUNGULIWA MASHITAKA NA FA WACHUNGUZA MASHABIKI KUINGIA UWANJANI WAKATI WA MECHI

Chama cha Soka England FA, kimeanza uchunguzi kuhusu Mashabiki wa Aston Villa kuvamia Uwanja kabla Mechi ya Uwanjani kwao Villa Park kati ya Aston Villa na West Bromwich Albion haijamalizika na pia mara baada ya kumalizika, Leo hii FA imetoa taarifa kuwa Kiungo wa WBA, Chris Brunt, amefunguliwa Mashitaka kwa kutoa lugha chafu kwa Waamuzi katika Mechi hiyo hiyo.
FA imedai kuwa Brunt alitoa lugha chafu kwa Mwamuzi mmoja wakati Mechi imekwisha na Wachezaji wapo kwenye njia ya kuelekea Vyumba vya Kubadili Jezi.
Brunt, mwenye Miaka 30, amepewa hadi Machi 12 kujibu Mashitaka yake.

Katika Mechi hiyo ya Robo Fainali, ambayo ni Dabi ya Midlands, Villa waliifunga WBA Bao 2-0 kwa Bao za Fabian Delph na Scott Sinclair na kuwafikisha Nusu Fainali ya FA CUP kwa mara ya kwanza tangu 2010. Mechi hiyo, licha ya Mashabiki kuvamia Uwanja na kusababisha isimame mwishoni kabla haijaendelea tena na kumalizwa na Refa, ilishuhudia Kadi Nyekundu 2 kwa Mchezaji wa Villa Jack Grealish na Claudio Yacob wa WBA. Uvamizi wa Mashabiki ulizuka tena mara baada ya Refa kumaliza Mechi hiyo na kuleta kashikashi kubwa ambayo FA imeanza kuifanyia uchunguzi.

No comments:

Post a Comment