Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini – TFF amepeleka
salamu za rambirambi kwa familia ya Bw. Nyama, kufuatia kifo cha mwamuzi
mstaafu Mohamed Nyama ambaye pia aliwahi kuwa mjumbe wa kamati ya waamuzi ya TFF kilichotokea jana kwao Nachingwea-
Lindi.
Marehemu Mohamed Nyama wakati wa uhai wake alikuwa mwamuzi
wa daraja la kwanza ambaye pia alitambuliwa na FIFA, Nyama anatarajiwa kuzikwa
leo jioni kwao Nachingwea mkoani Lindi na TFF itawakilishwa na Mjumbe wa Kamati
ya Utendaji Bw. Athumani Kambi.
Katika salam zake kwa familia ya Nyama, kwa niaba ya TFF,
familia ya mpira wa miguu na watanzania Rais Malinzi amewapa pole wapenzi wa
mpira wa miguu nchini katika kipindi
hiki kigumu cha maombelezo.
No comments:
Post a Comment