Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Friday, July 12, 2013

DROGBA KUJENGA HOSPITALI TANO IVORY COAST.

MSHAMBULIAJI wa zamani wa klabu ya Chelsea, Didier Drogba ametangaza kujenga hospitali tano nchini kwake Ivory Coast ili kuhudumia afya ya mama na mtoto.Taarifa hizo zilitolewa na katibu muhtasi wa Mfuko wa Didier Drogba, Guy Roland Tanoh jijini Abidjan mapema wiki hii. Tanoh amesema kiasi cha dola milioni tano zinatarajiwa kuwekwa katika mradi huo, huku kila hospitali ikijengwa katika miji mitano mikubwa ya nchi hiyo ambayo ni Abidjan, Yamoussoukro, Man, Korhogo na San Pedro.Tanoh amesema shughuli kwa ajili ya kuchangisha kiasi cha dola milioni 4 inatarajiwa kufanyika jijini London, Uingereza huku kiasi cha dola milioni moja kilichobakia kikitolewa na Drogba mwenyewe katika kuufanya mradi huo uwe wa kweli.

 

No comments:

Post a Comment