Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Friday, March 22, 2013

RAGE APOKELEWA KWA MABANGO AIRPORT, MASHABIKI NUSURA WAZICHAPE KAVUKAVU

Mabango yaliyobebwa na mashabiki waliofika uwanja wa ndege yakiwa na ujumbe mbalimbali

Rage akiwapungia mashabiki waliokuja kumlaki uwanja wa ndege

Mtu aliyevaa shati jeupe akipewa kichapo na mashabiki waliokuwepo uwanja wa ndege

Mashabiki wakisukuma gari la Rage baada ya kutokea gate la VIP
MWENYEKITI wa Simba Alhaj Aden Rage amerejea nchini akitokea India na kupokelewa kwa mabango yenye ujumbe mbalimbali yaliyokuwa yamebebwa na mashabiki wa timu hyo yenye makazi yake mitaa ya Msimbazi Kariakoo.

Ragw ambaye alitua majira ya saa 10.30 jioni na kushukia VIP alikuwa anasubiriwa na mashabiki wanaomuunga mkono huku wale ambao hawamkubali wakivurumishwa eneo hilo mara baada ya kufika.
eneo

Vijana hao wachache waliofika eneo wakiwa wamekunja mabango yao wakati wanaomuun ga mkono rage walifika wakiwa wameyaweka hadharani na kusomeka kwa kila mtu walikimbizwa hadi wakatolewa nje ya eneo la uwanja wa ndege

Baada ya kuwasili eneo hilo Rage aliwasalimia mashabiki hao na kuondoka nao hadi Kariakoo yalipo makao makuu ya Simba na kwenda kuwahutubia.

Awali akiwa uwanja wa ndege waandishi wa habari walimuuliza anasemaje kuhusu mapinduzi yaliyo na wanachama na yeye alisema hajui kama Simba kuna mapinduzi na kama yapo mbona amekuja kupokelewa na mashabiki.

Msafara wa mashabiki uliongozwa na Makamu Mwenyekiti mzee Kinesi na Afisa Habari Ezekiel Kamwaga na viongozo wengine

No comments:

Post a Comment