• Home
  • About Us
  • Contact Us

LENZI YA MICHEZO

MICHEZO NA BURUDANI


  • Home
    • MICHEZO
    • KITAIFA
    • SOKA
    • KIMATAIFA
    Home / Unlabelled / MPIGA GITAA WA MSONDO NGOMA AAGA DUNIA KUZIKWA LEO SAA SABA

    MPIGA GITAA WA MSONDO NGOMA AAGA DUNIA KUZIKWA LEO SAA SABA

    Rahel Pallangyo Thursday, January 24, 2013
     


    Marehemu Ismail Mapanga, enzi za uhai wake.

    MPIGA gitaa la besi wa bendi kongwe ya Msondo Ngoma, Ismail Mapanga, amefariki Dunia usiku wa kuamkia leo, katika Hospitali ya Temeke, jijini Dar es Salaam na kuacha pengo kubwa katika bendi hiyo.

    Akizungumza na Handeni Kwetu leo jijini Dar es Salaam, Meneja wa bendi hiyo, Said Kibiriti, alisema taarifa za msiba wa mwanamuziki ni nzito kwao, huku akitarajiwa kuzikwa leo saa saba mchana.

    Kibiriti alisema kifo cha Mapanga ni pigo kubwa kwa bendi yao, hasa kutokana na mchango wake katika tasnia ya muziki wa dansi, akiwa na Msondo Ngoma.



    Alisema wamepokea kifo hicho kwa masikitiko makubwa, huku wakiamini kuwa wameumizwa na msiba huo wa mpiganaji mwenzao, aliyewaacha wapweke.

    “Ni msiba mzito kwetu sisi wa Msondo Ngoma pamoja na wadau wote wa muziki wa dansi hapa nchini, ukizingatia kwamba marehemu ni kiungo mahiri mno.

    “Familia yake imeona azikwe leo saa saba mchana, huku mwili wake ukiwa nyumbani kwake Tandika, baada ya kufariki katika Hospitali ya Temeke, alipokuwa akisumbuliwa na maradhi ya tumbo,” alisema Kibiriti.

    Hata hivyo Kibiriti hakutaka kujibu swali la haraka ya mazishi ya mwanamuziki wake, hali inayoweza kuwanyima fursa ya kuzikwa na wadau na mashabiki wa Msondo kwa ujumla.

    Related Posts

    Post a Comment

    No comments

    Post a Comment

    Subscribe to: Post Comments ( Atom )

    MPIGANAJI

    MPIGANAJI

    WATEMBELEAJI

    Blogu Marafiki

    • BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE BLOG
      AL MASRY NAYO YATOLEWA KOMBE LA SHIRIKISHO AFRIKA - WENYEJI, CR Belouizdad wamefanikiwa kwenda Nusu Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika licha ya sare ya bila mabao na Al Masry usiku wa Jumamosi Uwanja wa N...
      4 hours ago
    • MICHUZI BLOG
      MAKAMU WA RAIS DKT NCHIMBI MGENI RASMI KILELE CHA MAADHIMISHO WIKI YA MAJI MKOANI MOROGORO - Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akisafiri kwa Treni ya Kisasa ya Umeme ya SGR kutoka Dar es Salaam kue...
      8 hours ago
    • BBC News Swahili
      'Nimemsamehe mpenzi wako aliyekuua' Barua ya mama kwa binti yake aliyeuawa - Mama yake Anne, Kate," anasema. "Je, tuendelee kuomboleza? Huzuni ni ya hakika. Lakini hatupaswi kubaki nayo," anasema.
      15 hours ago
    • HABARI NA MATUKIO
      Ayub Rioba Chacha Aaga Rasmi TBC Baada ya Miaka 10 ya Uongozi - *Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.* *Aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Tanzania Broadcasting Corporation (TBC), Ayub Rioba Chacha, ameaga rasmi watumishi wa s...
      18 hours ago
    • LENZI YA MICHEZO
      KIJANA SERIKALI HAIHITAJI KELELE INAHITAJI USHIRIKA WAKO - Katika ulimwengu wa sasa unaoendeshwa na matokeo, dhana ya kijana kukaa pembeni na kupiga kelele kuishtumu serikali inazidi kupitwa na wakati, badala ...
      1 day ago
    • CCM Blog
      RAIS SAMIA AWATAKIA EID MUBARAK - SALAMU ZA EID EL-FITRI Nawatakia Waislamu na Watanzania wote Sikukuu njema ya Eid el-Fitri. Tuyaishi na kuyaendeleza mema yote tuliyojifunza katika Mwe...
      1 day ago
    • MOBILA SAFARIS
      The Golden Circuit: A 7-Day Masterclass in Tanzanian Luxury - Tanzania is not just a destination; it is a sensory masterpiece. For those who seek the thrill of the wild without compromising on the refinements o...
      1 day ago
    • Wazalendo 25 Blog
      Uchukuzi : Naibu Waziri David Kihenzile Ashiriki Mkutano wa Kimataifa wa Masuala ya Uchukuzi Nchini Afrika Kusini - Naibu Waziri wa Uchukuzi David Kihenzile, ameshiriki Mkutano wa Kimataifa wa masuala ya Uchukuzi (NCT), mkutano uliofanyika katika Ukumbi wa Gallagher E...
      2 days ago
    • ZanziNews
      WAZIRI WA FEDHA AZINDUA MKUTANO WA MAPITIO YA SEKTA YA MAJI, ATAKA USHIRIKIANO KUIMARISHA HUDUMA NCHINI - Na Benny Mwaipaja, Morogoro. Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), amezindua rasmi Mkutano wa Mapitio ya Pamoja ya Sekta ya Maji (Joint Wa...
      3 days ago
    • HABARI MSETO BLOG
      -
    • WWW.BUKOBASPORTS.COM
      -
    Show 7 Show All

    TUFUATILIE

    • 200 Fans Like
    • 31,960 Followers Follow
    • 0 Fans Follow
    • 18 Subscribers Subscribe

    HABARI ZA MICHEZO PENDWA

    •  Mapinduzi ya Uchumi wa Kijani: Maombi 3,900 Yafungua Ukurasa Mpya wa Uwezeshaji Vijana Nchini
      Mapinduzi ya Uchumi wa Kijani: Maombi 3,900 Yafungua Ukurasa Mpya wa Uwezeshaji Vijana Nchini
      Kujitokeza kwa zaidi ya vijana 3,900 kuwania fursa za mtaji kupitia programu za Go Green na IMBEJU za CRDB Bank Foundation ni ishara tosha y...
    •  e-Utatuzi mkombozi kasi kukabili migogoro ya kazi Tanzania
      e-Utatuzi mkombozi kasi kukabili migogoro ya kazi Tanzania
      Safari ya mageuzi ya kidijitali nchini Tanzania imepiga hatua nyingine kubwa kupitia Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA), baada ya kuanzishwa...
    •  DIRA MOJA, TAIFA MOJA: SMT NA SMZ ZAUNGANISHA NGUVU MILANGO YA AJIRA NA MAHUSIANO YA KAZI
      DIRA MOJA, TAIFA MOJA: SMT NA SMZ ZAUNGANISHA NGUVU MILANGO YA AJIRA NA MAHUSIANO YA KAZI
        Katika kuonesha kielelezo cha juu cha mshikamano wa kidiplomasia na utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Serikali ya Jamhuri...
    •  TANESCO kuanza kukagua miundombinu ya umeme kwa ndege nyuki
      TANESCO kuanza kukagua miundombinu ya umeme kwa ndege nyuki
      Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limepiga hatua kubwa katika matumizi ya teknolojia baada ya kuzindua rasmi matumizi ya ndege zisizo na r...
    •  Mnyororo wa Thamani: Viwanda vya pamba na betri kumkomboa Mtanzania
      Mnyororo wa Thamani: Viwanda vya pamba na betri kumkomboa Mtanzania
      Serikali ya Tanzania imetangaza mkakati kabambe wa kugeuza mikoa ya kanda ya ziwa, hususan Simiyu, Shinyanga, na Mara, kuwa kitovu cha viwan...
    •  Tanzania yawasilisha hoja kimataifa uwekezaji sekta ya afya
      Tanzania yawasilisha hoja kimataifa uwekezaji sekta ya afya
      Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetoa hoja nzito katika jukwaa la kimataifa jijini London, Uingereza, ikitangaza utayari wake w...
    •  MKAKATI WA MATOKEO: KIWANDA KIPYA CHA TSN KULENGA GAWIO NA MASLAHI YA WATUMISHI
      MKAKATI WA MATOKEO: KIWANDA KIPYA CHA TSN KULENGA GAWIO NA MASLAHI YA WATUMISHI
      Serikali imebainisha kuwa kukamilika kwa kiwanda cha uchapaji cha Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) kutakuwa mhimili mkuu wa kiuchumi kw...
    •  ACHAGIZA AMANI NA MSHIKAMANO KATIKA FUTARI YA PAMOJA UKEREWE
      ACHAGIZA AMANI NA MSHIKAMANO KATIKA FUTARI YA PAMOJA UKEREWE
      Katika hafla ya futari ya pamoja iliyofanyika wilayani Ukerewe mkoani Mwanza, Mkuu wa Wilaya hiyo, Mheshimiwa Christopher Ngubiagai, ametoa ...
    •  Nyota wa Tembo Warriors Emmanuel Mlefu Atua Uturuki
      Nyota wa Tembo Warriors Emmanuel Mlefu Atua Uturuki
        Katika kile kinachoonekana kuwa ni muendelezo wa mafanikio makubwa kwa soka la walemavu nchini, mchezaji wa timu ya taifa ya Tembo Warrior...
    •  MAKAMU WA RAIS DK. NCHIMBI KUONGOZA MAADHIMISHO YA MIAKA MITANO YA HAYATI MAGUFULI CHATO
      MAKAMU WA RAIS DK. NCHIMBI KUONGOZA MAADHIMISHO YA MIAKA MITANO YA HAYATI MAGUFULI CHATO
      Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Emmanuel Nchimbi, anatarajiwa kuwa Mgeni Rasmi katika maadhimisho ya miak...

    Wasomaji Kimataifa

    Flag Counter

    MAKTABA YA MICHEZO

    BURUDANI GOFU HABARI JEZI JUDO KIKAPU KUOGELEA MICHEZO MICHEZO KIMATAIFA MICHEZO KITAIFA NGUMI RIADHA SANAA SOKA TAFF TFF WALEMAVU WANAWAKE

    KUMBUKUMBU ZA MICHEZO

    MARAFIKI

    HABARI MCHANGANYIKO

    HABARI MPYA

    HABARI ZINASOMWA ZAIDI

    • RATIBA NA MSIMAMO WA LIGI KUU TANZANIA BARA RAUNDI YA PILI, KAGERA SUGAR vs MBEYA CITY KUCHEZWA KAITABA STADIUM JUMAMOSI, YANGA VS ASHANTI UNITE TAIFA
      RATIBA NA MSIMAMO WA LIGI KUU TANZANIA BARA RAUNDI YA PILI, KAGERA SUGAR vs MBEYA CITY KUCHEZWA KAITABA STADIUM JUMAMOSI, YANGA VS ASHANTI UNITE TAIFA
      Mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara unaanza Jumamosi kwa mechi tano katika miji ya Bukob...
    • RATIBA LIGI KUU ENGLAND WIKIENDI HII NA MSIMAMO ULIVYO MPAKA SASA 2013/2014
      RATIBA Jumamosi 31 Agosti 14:45 - Manchester City v Hull City 17:00 - Cardiff City v Everton 17:00 - Newcastle United v Fulham 17:0...
    • HAWA NDIO MANCHESTER UNITED INAOWANYATIA KWENYE USAJILI LIGI KUU ENGLAND
      David Moyes is hoping for a more successful transfer window this time around Luke Shaw of Southampton ...

    Copyright (c) 2012 - 2025 LENZI YA MICHEZO All Right Reserved

    Designed by Gadiola Emanuel - 0784 643 633
    Template By TBN | Developed By Gadiola Emanuel