• Home
  • About Us
  • Contact Us

LENZI YA MICHEZO

MICHEZO NA BURUDANI


  • Home
    • MICHEZO
    • KITAIFA
    • SOKA
    • KIMATAIFA
    Home / Unlabelled / MPIGA GITAA WA MSONDO NGOMA AAGA DUNIA KUZIKWA LEO SAA SABA

    MPIGA GITAA WA MSONDO NGOMA AAGA DUNIA KUZIKWA LEO SAA SABA

    Rahel Pallangyo Thursday, January 24, 2013
     


    Marehemu Ismail Mapanga, enzi za uhai wake.

    MPIGA gitaa la besi wa bendi kongwe ya Msondo Ngoma, Ismail Mapanga, amefariki Dunia usiku wa kuamkia leo, katika Hospitali ya Temeke, jijini Dar es Salaam na kuacha pengo kubwa katika bendi hiyo.

    Akizungumza na Handeni Kwetu leo jijini Dar es Salaam, Meneja wa bendi hiyo, Said Kibiriti, alisema taarifa za msiba wa mwanamuziki ni nzito kwao, huku akitarajiwa kuzikwa leo saa saba mchana.

    Kibiriti alisema kifo cha Mapanga ni pigo kubwa kwa bendi yao, hasa kutokana na mchango wake katika tasnia ya muziki wa dansi, akiwa na Msondo Ngoma.



    Alisema wamepokea kifo hicho kwa masikitiko makubwa, huku wakiamini kuwa wameumizwa na msiba huo wa mpiganaji mwenzao, aliyewaacha wapweke.

    “Ni msiba mzito kwetu sisi wa Msondo Ngoma pamoja na wadau wote wa muziki wa dansi hapa nchini, ukizingatia kwamba marehemu ni kiungo mahiri mno.

    “Familia yake imeona azikwe leo saa saba mchana, huku mwili wake ukiwa nyumbani kwake Tandika, baada ya kufariki katika Hospitali ya Temeke, alipokuwa akisumbuliwa na maradhi ya tumbo,” alisema Kibiriti.

    Hata hivyo Kibiriti hakutaka kujibu swali la haraka ya mazishi ya mwanamuziki wake, hali inayoweza kuwanyima fursa ya kuzikwa na wadau na mashabiki wa Msondo kwa ujumla.

    Related Posts

    Post a Comment

    No comments

    Post a Comment

    Subscribe to: Post Comments ( Atom )

    MPIGANAJI

    MPIGANAJI

    WATEMBELEAJI

    Blogu Marafiki

    • MICHUZI BLOG
      MWENYEKITI UWT KIBAHA MJI ASHUSHA MAFUNZO YA KUJIKWAMUA KIUCHUMI KWA WANAWAKE KATA YA MSANGANI NA MKUZA - Na Victor Masangu, Kibaha Katika kupambana na wimbi la umasikini na kuachana na kuwa tegemezi kwa wanawake Mwenyekiti wa Jumuiya ya wanawake (UWT) Wilaya ...
      2 hours ago
    • HABARI NA MATUKIO
      Vodacom Tanzania yazindua kampeni ya "Zaidi ya Mtandao", Ikiimarisha dhamira yake ya kuleta fursa zaidi ya huduma za mawasiliano - *Mkurugenzi wa Biashara na Masoko wa Vodacom Tanzania Plc Brigita Shirima (katikati), Mkurugenzi wa Vodacom Business wa kampuni hiyo Nguvu Kamando (kulia...
      2 hours ago
    • CCM Blog
      WAKALA WA VIPIMO WAELEZA TIBA YA GESI PUNGUFU - *WANANCHI wametakiwa kuhakikisha wanapima mitungi ya gesi kabla ya kuinunua ili kujiridhisha kuwa wanapata kipimo cha gesi kinacholingana na fedha wana...
      3 hours ago
    • BBC News Swahili
      Nchi 10 zinazoongoza kwa uaminifu duniani na 10 zinazofanya vibaya zaidi - Watafiti walikabidhi jumla ya pochi 17,003 zilizodaiwa 'kupotea' kwa watu wanaosimamia biashara na taasisi mbalimbali, katika miji 355 na mataifa 40.
      7 hours ago
    • LENZI YA MICHEZO
      ENG: MARYPRISCA MAHUNDI: VIJANA TUJITOKEZE KUITETEA SERIKALI DHIDI YA UCHOCHEZI MITANDAONI - Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jinsia,Wanawake na Makundi Maalumu Eng. Maryprisca Mahundi amewataka vijana kusimama kusimama imara kukemea uchochezi na up...
      9 hours ago
    • Wazalendo 25 Blog
      Riadha : NMB Yamkabidhi Mwanariadha Alphonce Simbu Sh Milioni 10 Maandalizi ya Sydney Marathon Agosti 30 - Na Mwandishi Wetu, Arusha Benki ya NMB imekabidhi udhamini wa Sh10 milioni kwa mwanariadha wa Tanzania, Alphonce Simbu, ili kumsaidia katika maandalizi...
      1 week ago
    • MOBILA SAFARIS
      Royalty at Rest: Understanding the Silent Partnership of Serengeti Lions - There’s a quiet, undeniable beauty in the division of labor on the Serengeti Plains. While the lioness does the heavy lifting for the pride—driving...
      1 week ago
    • BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE BLOG
      YANGA SC YASAJILI CHIPUKIZI MWINGINE, NI HUSSEIN MIHAMBO WA MASHUJAA FC - KLABU ya Yanga imemtambulisha mshambuliaji chipukizi, Hussein Juma Mihambo (19) kutoka Mashujaa FC kuwa mchezaji wake mpya kuelekea msimu ujao. Anakuwa mc...
      2 weeks ago
    • ZanziNews
      WASIRA AWATOLEA UVIVU WALIOANZA MBIO ZA URAIS - MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Tanzania Bara, Stephen Wasira, Leo Machi 27, 2026, Mjini Bunda Mkoa wa Mara alipokuwa akiweka jiwe la ms...
      4 months ago
    • HABARI MSETO BLOG
      -
    • WWW.BUKOBASPORTS.COM
      -
    Show 7 Show All

    TUFUATILIE

    • 200 Fans Like
    • 31,960 Followers Follow
    • 0 Fans Follow
    • 18 Subscribers Subscribe

    HABARI ZA MICHEZO PENDWA

    Wasomaji Kimataifa

    Flag Counter

    MAKTABA YA MICHEZO

    BURUDANI GOFU HABARI JEZI JUDO KIKAPU KUOGELEA MICHEZO MICHEZO KIMATAIFA MICHEZO KITAIFA NGUMI RIADHA SANAA SOKA TAFF TFF WALEMAVU WANAWAKE

    KUMBUKUMBU ZA MICHEZO

    MARAFIKI

    HABARI MCHANGANYIKO

    HABARI MPYA

    HABARI ZINASOMWA ZAIDI

    Copyright (c) 2012 - 2025 LENZI YA MICHEZO All Right Reserved

    Designed by Gadiola Emanuel - 0784 643 633
    Template By TBN | Developed By Gadiola Emanuel