Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Tuesday, October 10, 2017

UCHAGUZI BODI YA LIGI KUFANYIKA JUMAPILI

Uchaguzi wa Kamati ya Uongozi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) unafanyika Jumapili, Oktoba 15 mwaka huu kwenye ukumbi wa mikutano wa Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
Wagombea saba wamepitishwa kuwania uongozi wa TPLB baada ya Kamati ya sasa kumaliza muda wote. Kamati mpya ya Uongozi itakayochaguliwa katika uchaguzi huo unaosimamiwa na Kamati ya Uchaguzi ya TFF utakaa madaraka kwa kipindi cha miaka minne.

Waliopitishwa kwenye kinyang’anyiro hicho baada ya orodha ya mwisho iliyotolewa Oktoba 9, mwaka huu ni Clement Andrew Sanga kutoka Yanga na Hamad Yahya Juma wa Mtibwa Sugar wanaowania uenyekiti wa TPLB.

Wengine ni Shani Christoms Mligo wa Azam FC ambaye ni mgombea pekee wa nafasi ya Makamu Mwenyekiti. Nafasi tatu za kuwakilisha klabu za Ligi Kuu kwenye Kamati ya Uongozi zimevutia wagombea wawili; Hamisi Mshuda Madaki (Kagera Sugar) na Ramadhani Marco Mahano (Lipuli).

Almasi Jumapili Kasongo kutoka Ashanti United FC ni mgombea pekee aliyejitokeza kuwania nafasi ya uwakilishi wa klabu za Ligi Daraja la Kwanza. Klabu za Daraja la Kwanza zina nafasi mbili.

Klabu za Ligi Daraja la Pili zina nafasi moja kwenye Kamati ya Uongozi ya TPLB, na mgombea pekee aliyejitokeza kuwania nafasi hiyo Edgar William Chibura kutoka Abajalo FC.

Jumla ya wajumbe 44 watashiriki Mkutano huo wa uchaguzi wa Baraza Kuu la TPLB. Wajumbe hao ni klabu 16 za Ligi Kuu, klabu 24 za Ligi Daraja la Kwanza na wawakilishi wanne wa klabu za Ligi Daraja la Pili.

Nafasi ya Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na wajumbe wa kuwakilisha klabu za Ligi Kuu zitapigiwa kura na klabu 16 pekee za Ligi Kuu.

No comments:

Post a Comment