Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, September 23, 2017

BANYAI:NILITISHIWA MAISHA NIKAAMUA KUJIUZULU



ALIYEKUWA kocha Mkuu wa Njombe Mji, Hassan Banyai amesema mashabiki wa timu hiyo walimtishia maisha ndio maana alilazimika kujiuzulu baada mchezo dhidi ya Mbeya City.
Akizungumza na wandishi wa habari Dar es Salaam Banyai alisema baada ya mchezo kumalizika kwenye Uwanja wa Sokoine Mbeya mashabiki hao walianza kumzonga Makamu Mwenyekiti  Emanuel Mbeyela na kuanza kutoa vitisho
“Baada ya kumaliza mchezo mashabiki walifanya kitendo ambacho siyo cha kiungwana cha kumfuata na kumzunguka Mwenyekiti wa timu Erasto Mpete na Makamu Mwenyekiti Emanuel Mbeyela baadae walinifuata kambini wakanikuta niko na wachezaji lakini hawakunidhuru,”
“Wakaniambia hii timu ni yetu na viongozi sisi ndio tumewaweka, tunakuomba kwa usalama wako usirudi Njombe ukiwa na timu maana tutakufanya chochote. Nilitafakari kwa kina na viongozi wakanipigia simu wakaniambia niondoke kambini maana siyo salama kwangu,” alisema Banyai.
Banyai alisema alilazimika kuhama hoteli aliyokuwa awali kwa ajili ya usalama wake na baadae akawasiliana Mpete na kumweleza azma yake ya kujiuzulu na kumkubalia na kumweleza kwa usalama wa maisha yake na familia ni bora akajiuzulu.
Lakini Banyai hakuishia hapo alisema baadhi ya viongozi wanamtupia lawama timu kufanya vibaya jambo ambalo anadai uongozi ndio wenye tatzo kwa sababu wakati timu inapanda ligi kuu alikabidhi ripoti lakini ripoti hiyo haikufanyiwa kazi.
“Niliikuta Njombe Mji ikiwa nafasi ya nne kwenye ligi daraja la kwanza lakini nilibadilisha timu na hatimaye ikapanda daraja, baada ya kupanda nilipendekeza namna nafasi za kufanyia usajili, kambi, vifaa, uwanja wa mazoezi na mechi za majaribio tano lakini kati ya vyote nilipata mechi za majaribio tu,”
Nilifika mahali nikachukua beeps zangu na kocha msaidizi akaleta zake na nililazimika kufanya mazoezi mara moja kwa siku kwa sababu uongozi ulisema hauna pesa na usajili wakafanya wanavyojua wao lakini baada nililazimika dakika za mwisho nililazimika kuongeza Ditrim Nchimbi, Awadh Juma na wengine wawili,” alisema Banyai
Banyai anasema sehemu waliyoweka kambi wakati wa maandalizi haikuwa rafiki kwa wachezaji kwani ilikuwa na mwingiliano mkubwa wa watu na kuzungukwa na kumbi za starehe jambo ambalo ni gumu kuwadhibiti wachezaji ukizingatia wachezaji wanapendwa na wanawake.
Pamoja na yote alishukuru uongozi wa timu hiyo kwani wamemlipa stahili zake zote na kuwatakia kila la heri katika ligi kuu.

No comments:

Post a Comment