Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, June 5, 2017

YANGA YATINGA NUSU FAINALI YA SPORTPESA BAADA YA KUIONDOA TUSKER FC KWA PENALTI





MABINGWA wa Ligi Kuu ya soka Tanzania bara,Yanga wametinga nusu fainali ya Kombe la SportPesa baada ya kushinda kwa penalti 4-2 dhidi ya mabingwa wa Kenya, Tusker.

Wakati Yanga wakishinda, watani wao, Simba watamenyana na Nakuru All Stars ya Kenya kesho katika mechi nyingine ya michuano hiyo. Mchezo wa Yanga ulifanyika katika Uwanja wa Uhuru na hadi dakika ya 90 zilikuwa suluhu.

Kwa matokeo hayo, Yanga itacheza nusu fainali na AFC Leopards ya Kenya keshokutwa. AFC Leopards iliitoa Singida United kwa penalti 5-4.

Kila timu iliyoingia nusu fainali imejinyakulia dola za Marekani 5,000 sawa na sh milioni 10. Waliofunga penalti za Yanga ni Nadir Haroub 'Canavaro', Obrey Chirwa, Maka Mwakaluka na Said Mussa. Kipa Deogratius Munishi alipangua penalti ya Clifford Alwanga.

Naye Stephen Owusu alipiga mpira juu ukagonga mwamba na kutoka. Walioifungia Tusker ni Noah Wafula na Brian Osumbe. Timu zote zilishambuliana kwa zamu. Yanga ilijaza vijana wengi wenye umri chini ya miaka 20.

Yanga: Deogratius Munishi, Nadir Haroub, Juma Abdul, Mohammed Nassor, Andrew Vincent, Pato Ngonyani, Yusuf Mhilu/Bakari Athumani, Maka Mwakalumwa, Obrey Chirwa, Juma Mahadhi/Samwel Greyson dk 90, Emmanuel Martin/Said Mussa dk 61.

Tusker: Ochenge Duncan, Collins Shivanchi, Martin Kiiza, Lloyd Wahome, James Situma, Ndawula Moses/ Noah Wafula dk 57, Antony Ndula/Brian Osumba dk 90, Humphrey Mieno, Michael Khamati/ Clifford Alwanga dk57, Allan Wanga na Abdul Hassan.

Singida United ilitolewa na AFC Leopards kwa penalti 5-4 baada ya kwenda sare 1-1 hadi dakika ya 90.
Singida United ilifunga katika dakika ya 10 kupitia Tafadzwa Kutinyu kwa kichwa baada ya kupokea mpira wa kona wa Simbarashe Nhivi.

AFC Leopards walisawazisha dakika ya 63 kupitia kwa Vincent Oburu. Kutokana na mechi hizo kuwa za mtoano, ilibidi penalti zipigwe.

Salum Chuku  alikosa penalti ya Singida United kwa kupaisha. Waliopata ni Atupele Green, Hamis Shango, Simbarashe na Muroiwa Elisha.

Wachezaji wa AFC Leopards, Mangoli Bernard, Marselas Ingots, Allan Katerega, Otieno Duncan na Gilbert Fiamengo wote walifunga.

Timu zilishambuliana kwa zamu na hadi mapumziko, Singida ilikuwa mbele kwa bao 1-0. Kipindi cha pili AFC Leopards walitawala mpira kwa asilimia kubwa huku Singida United ikionekana kuchoka mapema, wakasawazisha.

AFC Leopards inayofundishwa na Kocha Mtanzania, Denis Kitambi itacheza nusu fainali Ijumaa na Yanga.

Singida United: Elisha Muroiwa, Said Lubawa, Roland Msonjo, Hassan Dumba, Salum Chuku, Salum Ally, Wisdom Mtasa/Nizar Khalifan dk. 73, Tafadzwa Kutinyu, Atupele Green na Simbarashe Nhivi, Shango Hamis.

AFC Leopards: Andika Gabriel, Sikhai Dennis, Marcus Abwao, Salum Andallah, Ottieno Duncan, Whyvonne Isuza, Bernard Mangoli, Mawira Joshua, Gilbert Fiamenyo, Nyakha Haron/Allan Katerega dk 90 na Oburu Vincent/Marselas Ingots dk 90.

No comments:

Post a Comment