Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Tuesday, May 16, 2017

SERENGETI BOYS ILIPOILAZA MALI NA VIATU




TIMU ya soka ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17, Serengeti Boys jana ilianza vema michuano ya Afrika baada ya kuwabana mabingwa watetezi, Mali na kutoka nao suluhu.
Katika mechi hiyo iliyochezwa kwenye uwanja wa Stade de lAmitie mjini Libreville, Gabon Serengeti Boys ilianza kwa mashambulizi ya harakaharaka dakika za mwanzo za kipindi cha kwanza hali iliyowachanganya wachezaji wa Mali.
Timu hiyo inayoshiriki michuano hiyo ya Afrika kwa mara ya kwanza ilionekana kutotetereka dhidi ya mabingwa hao watetezi ambapo wachezaji wake walicheza kwa kujiamini zaidi mpaka mwisho wa mchezo huo huku safu yake ya ulinzi ikionekana kuwa imara zaidi.
Serengeti, ambayo sasa ina pointi moja, inajiandaa kucheza na Angola keshokutwa mechi ambayo ina nafasi ya kushinda.
Wawakilishi hao watacheza mechi ya mwisho Jumapili ya wiki hii dhidi ya Niger.
Timu nne za juu kwenye michuano hiyo zitafuzu kucheza fainali za kombe la Dunia kwa vijana zilizopangwa kufanyika India Oktoba mwaka huu, na hilo ndilo lengo la Serengeti Boys.
Akizungumza kwa njia ya simu muda mfupi baada ya mechi ya jana, kocha wa Serengeti Boys, Bakari Shime aliwashukuru wachezaji wake kwa kujiamini katika mechi hiyo.
Sasa hizo mechi nyingine zitakuwa rahisi kwetu kwa sababu tulichokuwa tunakitaka ni kutofungwa na bingwa mtetezi, vijana wetu wamejitahidi sana, Watanzania waendelee kutuamini tu, alisema.

No comments:

Post a Comment