Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Tuesday, May 16, 2017

MALINZI AELEZA KILICHOIPA USHINDI SERENGETI BOYS



Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Emil Malinzi ametoa siri ya uimara wa timu ya Tanzania ya vijana wenye umri wa chini ya miaka 17 akisema: “Haya yote kayafanya Dk. Harrison Mwakyembe.”
Akizungumza mjini Libreville, Malinzi amesema: “Ujumbe wa kuitakia kheri Serengeti Boys ulitolewa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo umeisukuma timu hiyo kufanya vema.
 “…Ndiyo, timu imekuwa ikijindaa physical, lakini kupata neno la mzazi kutoka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mheshimiwa Dk. John Magufuli kupitia Waziri wa Michezo, Mheshimiwa Mwekyembe liliwatia nguvu vijana kufanya vema na kuzuia Mali kuIshinda Serengeti.”
 Vyombo vya habari vya hapa Libreville, vimesema Serengeti Boys ni timu ya kuchungwa mara baada ya matokeo ya jana dhidi ya Mabingwa watetezi - Mali ambayo pia ni makamu bingwa katika Kombe la Dunia la FIFA kwa vijana chini ya miaka 17. 
Vyombo vya habari vya hapa vimesema ni matokeo mazuri na hata ya kushangaza kwani Mali ni timu ambayo hakuna timu inapenda kukutana nayo.
 “La kushangaza kwa timu ya Tanzania ambayo pamoja na Angola zina vijana wanaoonekana kuwa na umri mdogo kulinganisha na timu za Afrika Magharibi, ni uwezo wao wa kubaki kwenye mpango wa mchezo hata walipokumbana na mawimbi makali,” limesema gazeti la Le Moniour.
 Serengeti Boys imeanza kufuatiliwa na kuangalia matokeo yake ya mechi za nyuma na kuonekana imepoteza mechi chache za kimataifa na kuzifunga timu kama za Afrika Kusini, kutoka sare na Korea Kusini na Marekani katika michuano mbalimbali .

No comments:

Post a Comment