Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Wednesday, May 10, 2017

CAF YATAJA VIKOSI VYA TIMU ZA U-17 KWA FAINALI ZA MEI 14-28 GABON



SHIRIKISHO la Soka Barani Afrika limepitisha majina 21 ya wachezaji kwa Timu za Vijana ya Taifa waliochini ya miaka 17 ambayo zinashiriki Fainali za 12 Afika zinazotarajiwa kuanza Mei 14-28 nchini Gabon.
Katika taarifa iliyowekwa cafonline imetoa orodha ya wachezaji wa timu zote nane ambazo zinashiriki fainali hizo.
Pia taarifa hiyo inasema timu zitakazofuzu nusu fainali zitakuwa zimefuzu kuwakilisha Afrika katika fainali za FIFA U-17 zitakazofanyika nchini India kuanzia Oktoba 06-28 2017.
Katika orodha ya wachezaji waliopitishwa jina la mchezaji, jina la jezi, nafasi anayocheza, mwaka aliozaliwa na timu anayochezea.
Wakati  nchi zingine zinaonyesha timu ambazo wachezaji wao wanachezea ama wanatoka, wachezaji wa Tanzania wanaonekana hawana timu wanazochezea.
Kikosi cha Serengeti boys kilichopitishwa ni Ramadhan Kabwili, Ally Ng’anzi, Nickson Kibabage, Enrick Vitalis, Dickson Job, Issa Makamba, Cyprian Benedictor, Saidi Mussa na Abdul Suleiman
Wengine ni Assad Juma, Mohamed Rashid, Kibwana Ally, Shaaban Ada, Ally Msengi, Yohana Mkomola, Israel Mwenda, Ibrahim Abdallah, Samwel Edward, Muhsin Malima, Kelvin Kayego na Kelvin Nashon.



GONGA JINA LA NCHI KUTAZAMA KIKOSI CHAKE

Kundi A
Ghana

Kundi B

No comments:

Post a Comment