Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, December 10, 2016

YANGA YAKUBALI GWARIDE LA JKU MBELE YA WAZIRI WA MAMBO YA NDANI MWIGULU NCHEMBA









Yanga imejikuta ikichezeshwa gwaride na wanajeshi wa JKU baada kufungwa mabao 2-0 , katika mechi ya kujipima nguvu iliyochezwa kwenye uwanja wa Uhuru Dar es Salaam.
Hii ilikuwa mechi ya kwanza kwa kocha George Lwandamina tangu achukue mikoba kwa Hans van Pluijm aliyepelekwa nafasi ya Mkurugenzi wa Ufundi.
Mechi hiyo ni ya maandalizi ya mzunguko wa pili wa ligi unaotarajiwa kuanza kutimua vumbi Desemba 17 mwaka huu ambapo Lwandamina aliitumia kuangalia kikosi chake.
JKU ilipata bao la kwanza katika dakika ya 11 likifungwa na Emmanuel Martin kwa shuti kali baada ya kuunganisha mpira wa kona fupi kutoka kwa Feisal Salum.
Dakika ya 26 Martin aliifungia timu yake bao la pili kwa shuti kali ndani ya box baada ya kumzunguka beki wa Yanga Pato Ngonyani.
Katika mechi hiyo ya jana, Lwandamina alitumia vikosi viwili. Kikosi cha kwanza kilichokwenda mapumziko kikiwa nyuma kwa mabao 2-0 kilikuwa: Ally Mustafa 'Barthez', Hassan Kessy, Oscar Joshua, Pato Ngonyani, Nadir Haroub 'Cannavaro', Said Juma, Juma Mahadhi, Matheo Antony, Obrey Chirwa, Malimi Busungu na Geoffrey Mwashuiya.
Kikosi cha pili kilikuwa: Deogratius Munish, Juma Abdul, Haji Mwinyi, Vincent Bossou, Andrew Vincent, Justine Zulu, Deus Kaseke, Thaban Kamusoko, Donald Ngoma, Simon Msuva, Amis Tambwe na Deus Kaseke.
Hata hivyo kikosi hicho hakikubadi matokeo. Mchezaji Zulu ambaye wengi walitaka kumuona alionyesha kiwango kizuri kwani alikaba na kuchezesha timu ingawa ameonekana mzito.

No comments:

Post a Comment