Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, September 24, 2016

RASHFORD NA POGBA WAANZA KAZI MAN UTD IKIIFUNGA LEICESTER CITY 4-1

Kiungo  wa Manchester United, Paul Pogba (kulia) akikimbizwa na kiungo  wa Leicester City, Danny Drinkwater wakati wa mchezo wa Ligi Kuu ya England uliofanyika leo mchana kwenye Uwanja wa Old Trafford jijini Manchester, kaskazini magharibi ya London. Man United ilishinda mabao 4-1.


 
TIMU ya Manchester United leo imeutumia vizuri uwanja wake wa nyumbani wa Old Trafford baada ya kuwafunga mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya England Leicester City kwa mabao 4-1.

Wakati timu hiyo ikiibuka na ushindi mnono, kocha Jose Mourinho amemuacha kando ya kikosi cha kwanza nahodha wake Wayne Rooney.

Chris Smalling ndiye alikuwa wa kwanza kuipatia bao Man United kabla Juan Mata hajafunga la pili na kuifanya timu hiyo kuongoza kwa mabao 2-0.

Marcus Rashford na Paul Pogba  wamefunga mabao yao ya kwanza katika timu hiyo, ambapo yote yalifungwa kwa njia ya kona.

Mabingwa watetezi Leicester City wenyewe walipata bao lao la kufutia machozi lililofungwa na Demarai Gray kwa shuti la mbali.

Rooney aliingia uwanjani katika dakika ya 83.

No comments:

Post a Comment