Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, August 22, 2016

SERIKALI YAKABIDHIWA UWANJA WA UHURU

Katibu Mkuu wa wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo,Dokta, Elisante Ole Gabriel (kulia) akikikabidhiana nyaraka baada ya kukamilika ujenzi wa Uwanja wa Uhuru na  Meneja wa BCEG Ltd, Cheng Longhai,(kushoto) . Anayeshuhudia ni Waziri Nape Nnauye. (Picha na Rahel Pallangyo)



WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye, amesema serikali inawakaribisha wadau kuwekeza kwenye michezo makao makuu ya nchi Dodoma.
Nape aliyasema hayo wakati akikabidhiwa uwanja wa Uhuru na kampuni ya BCEG Ltd ambayo walikuwa wanaufanyia marekebisho ya kuuboresha na kuufanya kuwa wa kisasa.
"Mimi kama waziri mwenye dhamana ya michezo nawakaribisha wadau kuwekeza kwenye michezo hasa Dodoma ambapo serikali inahamia pia nawataka wadau kuutunza uwanja huu na kulipa ada za kuutumia", alisema Nape.
Pia Nape aliipongeza Azam kwa kumiliki uwanja wao huku akiziasa Simba na Yanga kukamilisha taratibu za ujenzi wa viwanja vyao ambao wamesema wanajenga.
Awali akikagua uwanja huo, Nape aliwaonyesha wandishi wa habari eneo ambalo serikali imetenga kwa ajili ujenzi wa ofisi wa vyama vya michezo kama walivyoomba kwa waziri mkuu alipokutana na kuzungumza na viongozi wa vyama vya michezo mara baada ya kuingia madarakani.
"Eneo hili michoro yake ipo tayari na lina ukubwa wa mita za mraba 4000 hivyo viongozi wanaweza kuja ofisini ili kupewa michoro wajenge kwa gharama zao, eneo hili ni kubwa kwani linaweza kujengwa baadhi ya ofisi za wizara", alisema Nape.
Awali akizungumza kabla ya kukabidhi uwanja huo, Meneja wa BCEG Ltd, Cheng Longhai, alisema uwanja huo ulianza kujengwa Mei 2015 na umegharimu bilioni 12.
Pia aliishukuru serikali kwa uaminifu na ushirikiano walioipa kampuni yake tangu kuanza kazi na kukamilisha.
Baada ya kukabidhiwa uwanja wa Uhuru, Nape alikwenda kukagua ujenzi wa mashine za elektroniki, uwanja wa Taifa kukiri kuridhishwa kazi na kasi ya mashine zenyewe kwani zitakuwa zinatumia sekunde 2 kwa mtu mmoja.
"Kazi hii inafanya na serikali na hii inatokana na ahadi ambayo niliitoa ya kudhibiti mapato ya kwenye michezo, kazi hii chini ya kampuni ya Selcom inaendelea vema na Septemba 4 watakabidhi rasmi", alisema Nape.
Pia Nape aliwatoa wasiwasi mashabiki kuhusu umeme kwenye mashine hizo kwani zimefungwa UPS ambayo inaweza kuhifadhi umeme zaidi ya saa tano lakini pia akawataka kujenga tabia ya kuwahi kuingia uwanjani kuepuka msongamano.
Jumla ya mashine 20 zinatarajiwa kufungwa Uwanja wa Taifa, 12 zitafungwa mageti ya mbele maarufu kama geti la Simba, mashine 6 na geti la Yanga mashine sita na mashine nane zitafungwa mageti ya nyuma kutokea uwanja wa ndani wa Taifa.

No comments:

Post a Comment