Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Thursday, May 12, 2016

BODI YA LIGI YAFAFANUA YANGA KUCHEZA NA NDANDA DAR

Mpaka sasa taarifa kutoka Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara (TPLB), mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, kati ya Ndanda na Young Africans umepangwa kufanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam mara baada ya Yanga kuomba hivyo na Ndanda kama timu mwenyeji kuridhia kuuhamisha kutoka Nangwanda Sijaona wa Mtwara.

Kwa nyakati tofauti, mwishoni mwa wiki iliyopita Young Africans ilituma maombi kwa Ndanda kadhalika TPLB kuomba ridhaa ya mchezo huo kufanyika Dar es Salaam kwa kuwa inatarajiwa kusafiri Jumapili alfajili kwenda Angola kwa ajili ya mchezo wa marudiano dhidia ya Sagrada Esperanca ya Angola.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka TPLB, Ndanda imekubali ombi la Young Africans iliyoomba mchezo huo uhamishwe kwa malengo ya kuisaidia Young Africans kuwahi usafiri ndege kwenda Angola ambako wanatarajiwa kucheza na wapinzani wao ama Mei 17 au 18, mwaka huu.

Barua ya Bodi ya Ligi kwa TFF imesema kwamba Young Africans watatumia mchezo huo ambao Ndanda itakuwa mwenyeji kupokea taji la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.

Ofisa Habari wa Yanga, Jerry Muro ameishukuru Ndanda kwa uungwana wao wa kujali maslahi ya taifa na kukubali mchezo huo kufanyika Dar es Salaam, kabla ya Young Africans kwenda Angola.

Kanuni ya pili ya Ligi Kuu Bara toleo la 2015/16 imeeleza wazi kuwa, “Katika mazingira maalumu, timu inaweza kucheza mchezo wake wa nyumbani katika uwanja mwingine endapo kuna sababu nzito na za msingi, utambulisho wa uwanja katika mazingira haya pia unawajibika kufanywa katika kipindi cha uthibitisho wa kushiriki ligi au kwa maombi maalumu kwa TPLB,” inasehemu kanuni hiyo.
Kwa kuzingatia kanuni hiyo na sababu za Yanga ambazo Ndanda na Bodi wameona kuwa ni nzito wamekubaliana kucheza mchezo huo Dar es Salaam.
Yanga inatarajiwa kucheza na wapinzani wao, Sagrada Esperanca ya Angola ama Mei 17 au 18, 2016. Katika mchezo wa kwanza ulifanyika Dar es Salaam Jumamosi iliyopita Yanga iliwafunga wageni wake mabao 2-1 katika mchezo uliofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Yanga inahitaji ama sare, ushindi na kama kufungwa basi si zaidi ya bao moja ili kuindoa Esperanca katika hatua ya awali, ili kuingia hatua ya makundi katika kusonga mbele.

No comments:

Post a Comment