Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, February 6, 2016

VITA YA DARAJA LA KWANZA KUWANIA KUPANDA LIGI KUU KUENDELEA LEO



 
VITA ya kuwania kupanda Ligi Kuu kwa timu za Kundi C inaendelea leo, ambapo Geita Gold FC itakuwa mwenyeji wa JKT Oljoro, mchezo ambao  unatabiriwa kuwa mgumu.
Mchezo huo utachezwa Shinyanga utavuta hisia za mashabiki wengi kwani timu ambayo itapoteza mchezo huo itajiweka kwenye wakati mgumu wa kupanda ligi Kuu.
Geita ina pointi 24 sawa na Polisi Tabora wakitofautiana kwa idadi ya mabao ya kufunga na kufunga inacheza na JKT Oljoro yenye pointi 22.
Endapo JKT Oljoro itashinda mchezo huo itaipita Geita kwa pointi moja kitendo ambacho kitasababisha michezo ya mwisho kuwa migumu.
Vita ya kupanda kwenye kundi C inajumuisha Polisi Tabora ambao wana pointi 24 ambao leo watakuwa wageni wa JKT Kanembwa yenye pointi tatu mchezo ambao utachezwa kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika.
Pia Polisi Mara itaikarisha Panone FC kwenye Uwanja wa Karume, Mara, mchezo ambao hauna msisimko kwani timu Panone wana pointi 15 na Polisi pointi 12 jambo linalowatoa kwenye mbio za kuwania kupanda daraja.
Kwenye kundi A, Ashanti United ambayo ina pointi 22 itacheza na KMC  FC yenye pointi 2, mchezo utakaochezwa Uwanja wa Karume, Dar es Salaam na African Lyon yenye pointi 23 wanaikarisha Polisi Dar yenye pointi 14 mchezo unaochezwa Uwanja wa Mabatini, Pwani.
Timu yoyote kati ya Ashanti United, KMC FC, African Lyon endapo itapoteza mchezo leo itajiweka pabaya kwenye mbio za kupanda Ligi Kuu msimu ujao.
Michezo mingine kundi A itachezwa kesho ambapo Friends Rangers itaialika Mji Mkuu, kwenye Uwanja wa Karume, Dar es Salaam na Kiluvya United dhidi ya Polisi Dodoma kwenye Uwanja wa Mabatini Pwani
Michezo mingine ambayo ni ya kukamilisha ratiba itakayochezwa leo ni ya kundi B, kwani Ruvu Shooting walishapanda ni kati ya Polisi Morogoro itakayoikaribisha Njombe Mji kwenye Uwanja wa Jamhuri Morogoro.
Kurugenzi FC wataikarisha JKT Mlale, Burkinafaso FC wataialika Lipuli FC na Kimondo FC wataikaribisa Ruvu Shooting, huko Vwawa Mbozi.

No comments:

Post a Comment