Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Friday, December 11, 2015

MALINZI APONGEZA UTEUZI WA NAPE



 
RAIS wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amemtumia salamu za pongezi mbunge wa jimbo la Mtama, Nape Nnauye kufuatia kuteuliwa kuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Wasanii na Michezo katika serikali ya awamu ya tano.
Akizungumza na gazeti hili, Malinzi alisema kuwa amempongeza Nape kwani TFF ina imani nae katika nafasi hiyo, na kuahidi kushirikiana katika michezo na haswa katika kusukuma gurudumu la maendeleo ya mpira wa miguu nchini.
“Sisi tuna imani nae hivyo nawaomba wanamichezo wampe sapoti ili aweze kutimiza majukumu yake kisawasawa. Pia nawapongeza wanamichezo wengine ambao wamechaguliwa katika nyadhifa mbalimbali katika chaguzi zilizofanyika na zinazoendelea”, alisema Malinzi
Malinzi amewapongeza Paschal Kihanga, Mwenyekiti wa chama cha soka Mkoa Morogoro kwa kuchaguliwa kuwa Meya wa manispaa hiyo, na James Bwire mmiliki wa shule ya Alliance kwa kuchaguliwa meya wa manispaa ya Nyamgana.
Amewatakia kila la kheri katika nafasi hizo walizozipata za kuwatumikia watanzania, na kwa niaba ya familia ya mpira wa miguu nchini anawaahidi kushirikiana nao.

No comments:

Post a Comment