Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Friday, December 18, 2015

JOSE MOURINHO AFUNGASHIWA VIRAGO NA CHELSEA, NANI KUSHIKA NAFASI YAKE KATI YA PEP GUARDIOLA, GUUS HIDDINK, BRENDAN RODGERS NA JUANDE RAMOS?

Mmiliki wa klabu ya Chelsea Roman Abramovich alikutana na bodi ya klabu hiyo kujadili hatima ya meneja wa klabu hiyo Jose Mourinho na sasa kuamua kumtimua.
Hii ni baada ya klabu hiyo kuandikisha matokeo mabaya sana msimu huu, matokeo ya karibuni zaidi yakiwa kuchapwa 2-1 na Leicester ligini Jumatatu.
Hiyo ilikuwa mara ya tisa kwa Chelsea kushinda Ligi ya Premia katika mechi 16 na sasa wamo alama moja pekee juu ya eneo la kushushwa daraja.

Mechi inayofuata kwa Chelsea ni Sunderland Jumamosi uwanjani Stamford Bridge.
Abramovich alitangaza kwamba bado alikuwa akimuunga mkono Mourinho Oktoba lakini matokeo hayajaimarika.
Abramovich na wenzake uongozini Chelsea wamekuwa wakimuunga mkono meneja huyo lakini kuna kizungumkuti cha matokeo mabaya na kuendelea kufanya vibaya Kwa Klabu hiyo kuimeifanya Imtimue Meneja wake na hii ni baada ya kutoimarika kwa Klabu hiyo.


Meneja wa Bayern Munich Pep Guardiola na Diego Simeone Atletico Madrid bado wana majukumu kwa sasa. Hili limepelekea uvumi kwamba sasa huenda Chelsea ikarudi tena kwa Guus Hiddink kwa mkataba wa muda.
Jose Mourinho hapa alioneka akiwa na Kikosi cha Chelsea siku ya Jumanne wakifanya mazoezi na leo hii Alhamisi Kutimliwa. Jose Mourinho amefukuzwa kama Meneja wa Chelsea Miezi 7 tangu awape Ubingwa wa Ligi Kuu England.
Mreno huyo mwenye Miaka 52 alikuwa Chelsea kwa kipindi chake cha pili baada ya kutwaa wadhifa wa Umeneja kwa mara ya Pili Juni 2013.
Msimu uliopita Chelsea ilitwaa Ubingwa ikiwa Pointi 8 mbele ya Man City lakini Msimu huu hali ni mbaya.
Wamefungwa Mechi 9 kati ya 16 za Ligi na wapo Nafasi ya 16 wakiwa Pointi 1 tu juu ya zile Timu 3 za mkiani.
Kipigo chao cha mwisho kilikuwa majuzi Jumatatu walipochapwa 2-1 na Leicester City wanaoongoza Ligi wakiwa Pointi 20 mbele ya Chelsea.
Warithi wa Mourinho wanatajwa kuwa Pep Guardiola, Guus Hiddink, Brendan Rodgers na Juande Ramos.

Mourinho sasa kuuangalizia Mtanange wa Chelsea dhidi ya Sunderland kwenye Tv

Mourinho amekuwa kwenye kizungumkuti baada ya Msimu huu Kikosi Chake kutofanya Vyema


Kipigo cha bao 2-1 kutoka kwa  Leicester jumatatu kiliongeza Machungu kwa Mmiliki na Wapenzi wa Soka wakiwemo Mashabiki wake.

Mourinho alisukumiza sababu kwa Wachezaji wake kuwa ndio waliosababisha katika Mechi hiyo lakini Mmiliki wa Klabu hiyo Bwana Roman Abramovich aliitisha Kikao na Sasa wameamua kumtimua Kiongozi huyo mwenye Makeke mengi na Majigambo mengi kwenye Soka.

No comments:

Post a Comment