Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, August 29, 2015

U-15 KUWAVAA NA KOMBANI YA MOROGORO

Timu ya taifa ya Vijana wenye umri chini ya miaka 15 (U15) leo inashuka dimbani kucheza na timu ya kombaini ya mkoa wa Morogoro (U15) katika mchezo wa kirafiki utakochezwa majira ya saa 10 jioni mjini Morogoro.
U-15 ambayo imeweka kambi ya takribani ya wiki moja mjini humo, imekuwa ikifanya mazoezi chini ya kocha wake Mkuu Bakari Shime ambaye amekuwa akiwaita vijana kila mwisho wa mwezi kwa ajili ya mazoezi na kucheza michezo ya kirafiki.
Mchezo huo wa kirafiki ni sehemu ya program ya timu ya vijana ya TFF, ambapo kocha anapata nafasi ya kuona maendeleo ya vijana wake baada ya kuwa wamefanya mazoezi na kuongeza vijana wengine katika kikosi hicho baada ya kuwa amerdhika na uweo wao katika michezo hiyo wanayocheza.
Timu hiyo ya U-15 inaandaliwa kwa ajili ya kuwania kufuzu kwa fainali za Mataifa Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17 zitakazofanyika nchini Madagascar mwaka 2017.
U-15 wanatarajiwa kucheza michezo miwili na kombaini ya mkoa wa Morogoro leo jumamosi na kesho jumapili, kabla ya kuvunja kambi na vijana kurejea makwao na kukutana tena mwishoni mwa mwezi Septemba kwa ziara ya mkoa mwingine.

No comments:

Post a Comment