Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, August 22, 2015

MAN U YABANWA NA NEWCASTLE LEO


TIMU ya Manchester United leo imetoka suluhu na Newcastle United katika mchezo wa Ligi Kuu ya England uliofanyika kwenye Uwanja wa Old Trafford.

Bao lililofungwa na Wayney Rooney lilikataliwa na mwamuzi kwa madai kuwa mfungaji alikuwa ameotea baada ya kuwa nyuma ya mabeki wa Newcastle United.

Aleksandar Mitrovic, akicheza kwa mara ya kwanza katika kikosi cha Newcastle, nusura aipatie bao timu hiyo baada ya kupiga shuti lililogonga mwamba kabla ya Javier Hernandez mpira wake kuzuiwa na Krul na Chris Smalling kugonga mwamba katika muda wa majeruhi.

Matokeo hayo yana maana kuwa wenyeji Man United bado hawajafungwa na hawajaruhusu bao lolote kutinga katika wavu wao katika mechi za ligi msimu huu.

Louis van Gaal alimuanzisha Schweinsteiger, ambaye baadaye alitoka na nafasi yake kuchukuliwa na Michael Carrick wakati Newcastle ilifanya mabadiliko mara tatu kutoka katika kikosi kilichoifunga Swansea.

No comments:

Post a Comment