Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, July 25, 2015

MKURUGENZI LORD HARRIS AMUUNGA MKONO ARSENE WENGER

Mkurugenzi wa Arsenal, Lord Harris, amesema Meneja wao Arsene Wenger anaungwa mkono kiasi kuwa na uwezo wa kununua Mchezaji yeyote anaemtaka Duniani.
Baada ya kuwa na hali mbaya Kifedha baada ya ujenzi wa Uwanja wao mpya Emirates, Lord Harris amedai sasa wana uwezo wa Kifedha wa kununua karibu Mchezaji yeyote Duniani.
Amesema: "Tutamuunga mkono kuvunja Rekodi ya Klabu ya Ununuzi wa Mchezaji. Akimtaka Mchezaji, atampata. Ukiwaondoa Lionel Messi na Cristiano Ronaldo, anaweza kumchukua Mchezaji yeyote yule."

Wenger, ambae yupo Arsenal kama Meneja tangu 1996, ameiongoza Arsenal kutwaa Ubingwa wa Ligi Kuu England mara 3 na kutwaa FA CUP mara 5.
Lakini alikaa Miaka 9 bila ya Kikombe chochote hadi 2014 na 2015 alipobeba FA CUP mara 2 mfululizo.
Karim Benzema ni moja ya mchezaji anayetakiwa na Kocha huyoPetr Cech

No comments:

Post a Comment