Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, June 27, 2015

YANGA YATOKA SARE NA SPORT CLUB VILLA JOGOO YA UGANDA TAIFA






HUKU ikishuhudiwa na wachezaji na wachezaji wake wa kigeni Donaldo Ngoma na Joseph Tetteh Zutah waliowasili Dar es Salaam leo, Yanga ilijukuta ikitoka sare ya bila kufunga na Sports Club Villa ya Uganda kwenye mchezo wa kirafiki uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Kwenye mechi hiyo maalumu kwa ajili ya kupinga mauji ya albino na mgeni rasmi kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Saidi Mecky Sadiki, Yanga ilipoteza nafasi nyingi za kufunga kwenye mchezo huo.
Washambuliaji wa Yanga wakiongozwa na Amisi Tambwe na Simon Msuva walishindwa kufurukuta mbele ya ukuta thabiti wa Sports Club Villa ambao ni mabingwa wa Uganda.

Yanga iliwachezesha wachezaji wake wapya iliowasajili msimu huu kama vile winga Deus Kaseke aliyetoka Mbeya City, Malimi Busungu aliyetoka Mgambo JKT na chipukizi Godfrey Mwashuiya aliyesajiliwa wakati wa dirisha dogo walishindwa kabisa kuipenya na kushuhudia wakipoteza nafasi kadhaa za kufunga hasa kipindi cha kwanza.

Malimi Busungu alikosa bao la wazi kwenye dakika ya 31 baada ya kupokea pasi nzuri ya winga Goefrey Mwashuiya, lakini mpira aliopiga ulitoka pembeni kidogo ya Yanga la Sports Club Villa na dakika ya 39 Amis Tambwe alikosa bao la wazi akiwa ambeki peke yake na kipa wa Villa Sebweto Nicholaus.

Kwenye mechi hiyo timu zote zilifanya mabadiliko kadhaa kwa Yanga kuwapumzisha Malimi Busungu na kumuingiza Kpah Sherman na Nadir Haroub’Cannavaro’ alitoka baada ya kuumia na kuingia Pato Ngonyani.

Huku Villa ikiwatoa Kasule Abdulkarim na kumuingiza Dua Abeid na kisha kumtoa Kazibente James na kumuingiza Kamazi Dennis.
Hata hivyo Yanga walipata penalti kwenye dakika ya 79 baada ya Deus Kaseke kuangushwa kwenye eneo la hatari lakini Simon Msuva alipaisha penalti hiyo na kuinyima Yanga ushindi kwenye mechi hiyo ya kujipima nguvu kujiandaa na mashindano ya kombe la Kagame.

Yanga mpaka sasa imecheza michezo miwili ya kujipima nguvu ambapo wiki hii iliifunga klabu ya daraja la kwanza ya Friends Rangers kwa mabao 3-2 kwenye mechi iliyochezwa kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume.

No comments:

Post a Comment