Waziri mkuu nchini Morocco Abdelilah Benkirane ameamrisha kufanywa
uchunguzi kuhusu matangazo ya runinga ya tamasha ya mwanamuziki Jennifer
Lopez.
Tamasha hiyo inayofahamika kama Mawazine iliandaliwa mjini
Rabat tarehe 29 mwezi Mei na kupeperushwa na kituo cha runinga cha 2M.Bwana Benkirane amesema picha kutoka kwa tamasha hilo zilikuwa potovu na kuongeza kuwa matangazo hayo yalikiuka sheria za matangazo ya picha za nchi hiyo.

Akimuandikia barua rais wa halmashauri ya matangazo ya redio na runinga nchini Morocco , bwana Benkirane alitaka halmashauri hiyo kuwachukulia hatua za kisheria wale waliohusika.

Nalo kundi linalohusika na elimu la TMZ linasema kuwa linamshtaki mwimbaji huyo kwa kuwa Lopez ameshusha hadhi ya wanawake.
No comments:
Post a Comment