Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Wednesday, June 24, 2015

COASTAL UNION YAMNASA MAYANJA WA KAGERA SUGAR



UONGOZI wa Coastal Union,Wagosi wa Kaya umeingia mkataba wa miaka miwili na aliyekuwa Kocha Mkuu wa Kagera Sugar, Jackson Mayanja kuifundisha timu ya Coastal Union katika msimu ujao wa Ligi kuu soka Tanzania Bara itakayoanza Mwezi Agosti mwaka huu .
Kocha huyo ambaye ni raia wa Uganda, ameingia karandasi ya kuinoa Coastal Union leo jijini Tanga mbele ya Katibu Mkuu wa timu hiyo, Kassim El Siagi na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji Albert Peter.
Akizungumza kwa njia ya simu baada ya kumalizika zoezi hilo,Ofisa Habari wa Coastal Union,Oscar Assenga amesema kuwa kutokana na umahiri aliokuwa nao kocha huyo wana imani ataipa mafanikio timu yao katika ligi kuu msimu ujao.
“Uwezo wa kocha Mayanja unatupa matumaini makubwa ya mafanikio ukizingatia ana  uwezo wa kufundisha na kupata mafanikio hivyo tunaamini kuja kwake kwetu itakuwa chachu katika maendeleo”, alisema Assenga
Mayanja aliwahi kuzifundisha timu za soka Kiyuvu FC ya Rwanda,timu ya Mamlaka ya Mapato (URA),Vipers  FC ya Bunamwaya  na KCC zote za Uganda amesema kutua kwake kwenye timu Coastal Union kunampa faraja hivyo atahakikisha anatoa mchango wake kuipa mafanikio.
Pia alisema mipango yake ni kuhakikisha timu inang’ara katika michuano ya ligi kuu msimu ujao ikiwa ni pamoja na kubadili aina ya mchezo wa timu hiyo ili iweze kupata mafanikio kwa kuhirikiana na wachezaji, mashabiki na uongozi kwenye medani za kitaifa na kimataifa.

No comments:

Post a Comment