Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, December 13, 2014

REAL MADRID, MWAKA WA REKODI MPYA RONALDO ACHEKA UGENINI, AFUNGA BAO MBILI REAL MADRID IKIIFUNGA UD ALMERIA 4-1 LIGI YA LA LIGA

Real Madrid Jana wamepata ushindi wao wa 20 mfululizo katika Mashindano yote huku Cristiano Ronaldo akipiga Bao 2 wakati walipoifunga Ugenini Almeria Bao 4-1 katika Mechi ya La Liga. 

Real wameshinda Mechi zao zote kuanzia Septemba 13 na wapo Mechi 4 nyuma ya Rekodi ya Dunia ya kushinda Mechi 24 mfululizo iliyowekwa na Klabu ya Brazil Coritiba Mwaka 2011.
Hadi Mapumziko, Real walikuwa mbele kwa Bao 2-1 kwa Bao za Isco na Gareth Bale Kwenye Mechi hiyo, Kipa Iker Casillas aliokoa Penati iliyopigwa na Verza. 

Kipindi cha Pili Real walipiga Bao 2 nyingine kupitia Ronaldo na kushinda Bao 4-1. 
Hivi sasa Ronaldo amefunga Jumla ya Mabao 32 kati Mechi 23 na kwenye La Liga ana Bao 25 katika Mechi 14.
Juzi Jumanne, Real walivunja Rekodi ya Barcelona ya kushinda Mechi 18 mfululizo walipoifunga Lugorets kwenye Mechi yao ya mwisho ya Kundi lao la UEFA CHAMPIONS LIGI. 

Mechi hii ya La Liga na Almeria ni ya mwisho kwa Real kwa Mwaka huu kwa vile wao wanasafiri kwenda Nchini Morocco kucheza Mashindano ya FIFA ya Kombe la Dunia kwa Klabu yaliyoanza Desemba 10 na wao wakiwa Wawakilishi wa Ulaya kama Klabu Bingwa.
wamebeba Makombe ya UEFA CHAMPIONS LIGI na Copa del Rey. Hivi sasa Real wapo Pointi 5 mbele ya Barcelona kwenye La Liga.

LA LIGA
RATIBA/MATOKEO
Ijumaa Desemba 12 

UD Almeria 1 Real Madrid CF 4

Jumamosi Desemba 13 
18:00 Getafe CF v FC Barcelona
20:00 Valencia C.F v Rayo Vallecano
22:00 Cordoba CF v Levante

Jumapili Desemba 14 
0:00 Malaga CF v Celta de Vigo
14:00 RCD Espanyol v Granada CF
19:00 Sevilla FC v SD Eibar
21:00 Atletico de Madrid v Villarreal CF
23:00 Real Sociedad v Athletic de Bilbao

Jumatatu Desemba 15 
22:45 Deportivo La Coruna v Elche CF

Ijumaa Desemba 19 
22:45 Celta de Vigo v UD Almeria

No comments:

Post a Comment