Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Friday, December 26, 2014

MANCHESTER UNITED ITAWEZA KUWAPA ZAWADI YA BOXING DAY DHIDI YA NEWCASTLE, OLD TRAFFORD LEO

MANCHESTER UNITED ndio Wafalme wa Boksing Dei huko England katika Historia ya Ligi Kuu England kwa kuweza kushinda Mechi 19, kupoteza Mechi 1 tu katika Mechi 22 walizocheza Siku hiyo Desemba 26 na safari hii, Siku hiyo hiyo, watakuwa kwao kucheza na Newcastle.

Wakati Man United wakitawala Boksing Dei, Newcastle ni goigoi Siku hiyo kwa kushinda Mechi 4 tu katika Miaka 20 ya Ligi Kuu England na safari hii wanakutana na Man United, ambayo ipo Nafasi ya Tatu kwenye Ligi baada ya wimbi la kutofungwa katika Mechi 7 ambazo wameshinda 6 na Sare 1, wanaoingia Old Trafford wakiwa wamepewa Ofu Siku ya Krismasi na Meneja wao Louis van Gaal kitu tofauti na Timu nyingine ambazo hufanya Mazoezi Siku hiyo kwa ajili ya Mechi za Siku ya Pili
Kocha wa Newcastle Pardew ataiongoza timu yake ya Newcastle ugenini leo huko Old Trafford Manchester Kipa wa United David De Gea anatarajia kulinda lango la Man United leo, Mchezo utakaopigwa jioni saa 12.Kocha wa Newcastle

No comments:

Post a Comment