Ofisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB), Silas Mwakibinga
amemaliza mkataba wake tangu Oktoba 31 mwaka huu.
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na
TPLB wanamshukuru Mwakibinga kwa mchango wake kwa kipindi ambacho ameitumikia
Bodi, na kumtakia kila la kheri katika majukumu yake mapya huko aendako.
TPLB hivi sasa iko katika mchakato wa kupata
Ofisa Mtendaji Mkuu mpya kwa ajili ya kuziba nafasi hiyo iliyoachwa wazi na
Mwakibinga baada ya muda wa mkataba wake kumalizika.
No comments:
Post a Comment