Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Tuesday, October 28, 2014

CAPITAL ONE CUP LEO MECHI 5 KUCHEZWA, LIVERPOOL vs SWANSEA, SHREWSBURY vs CHELSEA

CAPITAL ONE CUP, ambalo ndio Kombe la Ligi, leo na kesho Usiku linaingia Raundi ya 4 kwa Mechi 8.

Leo Usiku zipo Mechi 5 ambazo ni pamoja za Vigogo Chelsea kucheza Ugenini na Shrewsbury, Timu ya Daraja la Ligi 2 ambalo ni Madara matatu chini ya Ligi Kuu, wakati Liverpool watakuwa kwao Anfield kucheza na Swansea City, pambano linalohusisha Timu za Ligi Kuu England pekee.
Jumatano yapo mapambano mawili ya Timu za Ligi Kuu England pekee ambayo ni huko Etihad kati ya Mabingwa wa England na Mabingwa Watetezi wa Kombe hili, Man City, dhidi ya Newcastle, na jingine ni lile la Stoke City v Southampton.

Siku hiyo hiyo, Tottenham watakuwa kwao White Hart Lane kucheza na Brighton City ambayo inacheza Daraja la Championship ambalo ni chini tu ya Ligi Kuu England.

Washindi wa Raundi hii ya Nne watatinga Robo Fainali ambayo Droo yake itafanyika kesho kutwa na Mechi zake kuchezwa Wiki ya Desemba 14.
CAPITAL ONE CUP
RAUNDI YA 4
RATIBA
Jumanne Oktoba 28

22:45 Bournemouth v West Brom
22:45 MK Dons v Sheffield United
22:45 Shrewsbury v Chelsea
2300 Fulham v Derby
2300 Liverpool v Swansea

Jumatano Oktoba 29
22:45 Man City v Newcastle
22:45 Stoke v Southampton
22:45 Tottenham v Brighton


FAINALI
Jumapili 1 Machi 2015

No comments:

Post a Comment