Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, September 20, 2014

Suso wa Liverpool kujiunga na AC Milan Januari

Nyota kinda wa Liverpool  Suso ameripotiwa kukubali kujiunga na kigogo cha soka nchini Italia AC Milan kwa uhamisho wa kudumu huku swali likisalia kuwa ni lini mchezaji huyo mhispania kijana ataelekea Rossoneri.
Suso, ambaye amekuwa katika kikosi cha kwanza cha Liverpool mara 14 alijiunga Anfield mwaka 2010, amekubali kuingia kandarasi ya miaka minne mkataba wenye thamani ya pauni £1.2 kwa mwaka hii ikiwa ni kwa mujibu wa habari kutoka nchini Italia.
Kijana huyu raia wa Hispania amekuwa mchezaji huru tangu kumalizika kwa mkataba msimu uliopita huku taarifa zaidi zikisema kuwa Milan wanajipanga kukamilisha usajiliwa kiungo huyo mshambuliaji mwezi Januari.

No comments:

Post a Comment