Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Wednesday, September 17, 2014

REAL MADRID YAIFUNGA BASLE MABAO 5-1 CHAMPIONS LEAGUE

Wachezaji wa Real Madrid Gareth Bale na Cristiano Ronaldo wakipongezana baada ya kuifunga Basle bao 4-1 katika kipindi cha kwanza cha dakika 45.Dakika ya 14 Real Madrid walijipatia bao la kwanza la kujifunga wao wenyewe Basle kupitia kwa Marek Suchy.

Dakika ya 30 Gareth Bale aliwachoma bao la 2 Basle na kufanya 2-0 baada ya kupata mpira kutoka kwa Luka Madrick. Dakika ya 31 C. Ronaldo alipachika bao la tatu na kufanya 3-0 baada ya kupewa pasi na Gareth Bale. Dakika ya 37 James Rodríguez alipachika bao la 4. Nao Basle walipata bao dakika ya 38 kupitia kwa Derlis González baada ya kutanguliziwa mbele pasi na Luca Zuffi.

Bao la tano lilifungwa na Karim Benzema baada ya kupewa mpira na Cristiano Ronaldo katika dakika ya 78 kipindi cha pili.

No comments:

Post a Comment