Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, September 13, 2014

FRANCIS JOHN KINAULANGA AIBUKA DEREVA BORA WA MWAKA WA SCANIA

. Mnadhimu Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Johansen Kahatano (kushoto) akimkabidhi  kombe dereva  Francis John Kinaulanga (kulia) baada ya kuibuka dereva bora wa mwaka 2014 wa shindano la scania ”Scania Driver of the year competition 2014” lililofanyika katika Viwanja vya Tanganyika Parkers, Kawe jijini Dar es Salaam. (Picha na Rahel Pallangyo)

Mshindi wa shindano la Scania Scania Driver of the year competition 2014”  Francis John Kinaulanga (katikati) akiwa na mshindi namba mbili Ramadhani Ahmad Danga (kulia) na Winston Rwegalulila Rwechungura (kushoto) baada ya kutangazwa washindi kwenye Viwanja vya Tanganyika Parkers, Kawe jijini Dar es Salaam.

Washiriki wa shindano wakiwa kwenye picha ya pamoja


Mshindi wa pili akiwa na zawadi zake



Shindano hili ambalo lilivuta umati mkubwa wa watu japo kulikuwepo mvua za hapa na pale lilifanyika katika viwanja vya Tanganyika Parkers, Kawe jijini Dar es Salaam leo.
Nafasi ya pli ilichukuliwa na Ramadhani Ahmad Danga na nafasi ya tatu ilikwenda kwa Winston Rwegalulila Rwechungura ambao wote kwa pamoja walipata nafasi ya kwenda nchini  Afrika Kusini  kushiriki faibnali za Scania ambazo zitahusisha madereva wan chi zilizo kusini mwa jangwa la Sahara.
Akizungumza wakati akikabidhi  zawadi kwa washindi, Mnadhimu Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Johansen Kahatano aliwapongeza madereva alishinda na kuwataka kuwa mfano bora kwa utii wa sheria barabarani.
“Nawapongeza madereva wote kwa kushiriki shindano hili lakini kipekee kwa washindi watatu wa mwanzoni na naowaomba muwe mabalozi wazuri wa utii wa sheria barabarani si kwamba muishie hapa kwenye shindano”, alisema Kahatano.
Pia aliipongeza kampuni ya Scania kwa kuendesha shindano  hili kwani litaibua hari kwa madereva wengine kushiriki na kuwa chachu wa utii wa sheria za barabarani jambo ambalo litaepusha ajali za barabarani ambazo zinazepukika.
Naye Afisa mwendeshaji wa Scania Kisali Nnyari, alisema kuwa washndi watatu wa juu watagharamia safari ya kwenda nchini Afrika Kusini wao na wenzao wao pamoja na bosi wa kampuni yake kwa siku saba kuanzia malazi, chakula na usafari wa kwenda na kurudi.
Sehemu ya umati uliofika kushuhudia
Shindano hili linafanyika kwa mara ya pili hapa nchini na limeacha gumzo kwa watu waliojitokeza kushuhudia huku madereva wengine wakiomba kuingizwa kwenye orodha ya washiriki bila kupitia hatua za awali jambo ambalo lilishindikana kukutokna na sheria za shindano lenyewe.


No comments:

Post a Comment