Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Tuesday, June 17, 2014

WORLD CUP 2014: GHANA 1 v UNITED STATE 2, CLINT DEMPSEY AWEKA HISTORIA...AFUNGA BAO LA MAPEMA..SEKUNDE 29! JOHN BROOKS AKIWAFUNGIA U.S BAO LA USHINDI!!

John Brooks alifunga Bao la Kichwa Dakika 4 kabla Mpira kumalizika na kuipa USA ushindi wa Bao 2-1 kwenye Mechi ya Kundi G iliyochezwa huko Estadio das Dunas Jijini Natal Nchini Brazil. 
USA walitangulia kupata Bao Sekunde ya 29 tu, hili likiwa ni Goli la 5 la mapema kwenye Historia ya Kombe la Dunia, alilofunga Clint Demsey, Mchezaji wa zamani wa Fulham. 
Andre Ayew aliisawazishia Ghana Dakika ya 82 baada kupokea Pasi ya Kisigino ya Asamoah Gyan.
Biashara mapema: Clint Dempsey akishangilia vikali baada ya kuifunga Ghana bao la baridi...mapeeema!!
Dempsey akiruka juu baada ya kuziona nyavu za Ghana hapa Natal
 Dempsey akipongezwa na wenzake kwenye kona ya uwanja..
Mashabiki wa USA wakishangilia kwa aina yao...Scarf juu
Dempsey ilikuwa kama sekunde 29 mpaka 31 kitu 1-0
Dada akishindwa kujizuia...yeye na USA damu damu
Rasta!! akipandwa na mizuka ya Ghana wakati wanaumana na  USA usiku huu
 Dempsey akifurahia bao ..wachezaji wa akiba walishindwa kuamini ..bao hilo!!
United State wameweka Historia katika Mtanange huu pale wapojichukulia pointi tatu muhimu. Dakika ya kwanza tuu Clint Dempsey alipoipachikia bao la kwanza United State kwa kufanya 1-0 dhidi ya Ghana baada ya mabeki kukaangwa mpaka ndani ya himaya yao na kuachia shuti kumfunga kipa Kwarasey, Akipewa pasi na Jermaine Jones. Kipindi cha pili dakika 82 André Ayew aliisawazishia Ghana na kufanya 1-1 baada ya kupewa pasi safi na Asamoah Gyan. Lakini muda mchache baadae United State waliongeza bao la ushindi kupitia kwa John Brooks baada ya kupigwa kona na hatimaye John Brooks kujitwisha mpira huo na kufunga bao la kichwa katika dakika ya 86 mpiga kona hiyo akiwa ni Graham Zusi.
Howard akipangua mpira langoni mwake dhidi ya adui.Historia tayari....Clint Dempsey akishangilia..Mchezaji wa United States Clint Dempsey akishangilia bao lake la mapeema dakika ya kwanza.Mchezaji wa United States Clint Dempsey akiifunga bao Ghana usiku huu, Bao likiwa ni la haraka haraka katika dakika ya kwanza.
Dempsey akishangilia bao lake la kwanza..dhidi ya Ghana
Dakika ya kwanza tuu Clint Dempsey anaipachikia bao la kwanza United State kwa kufanya 1-0 dhidi ya Ghana baada ya mabeki kukaangwa mpaka ndani ya himaya yao na kuachia shuti kumfunga kipa Kwarasey, Akipewa pasi na Jermaine Jones. United State kulipa kisasi usiku huu!??
VIKOSI:
Ghana starting XI
Ghana (4-2-3-1):Kwarasey, Gyan, Opare, Atsu, A. Ayew, Muntari, J. Ayew, Rabiu, Mensah, Asamoah, Boye
USA starting XI
USA (4-4-2):Howard, Bradley, Besler, Beasley, Dempsey, Bedoya, Jones, Beckerman, Altidore, Cameron, Johnson.Mashabiki pande zote mbili...

No comments:

Post a Comment