Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Sunday, May 25, 2014

VURUGU ZATAWALA KATIKA NGUMI MSHINDI ASHINDWA KUTANGAZWA

Bondia Said Mbelwa kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Karama Nyilawila wakati wa mpambano wao wa ubingwa wa UBO uliofanyika katika ukumbi wa frends corner manzese Dar es salaam hata hivyo mshindi ajapatikana kutokana na fujo zilizotokea katika raundi ya nane
Bondia Zumba Kukwe kushoto akioneshana umwamba na Josef Njelekela wakati wa mpambano wao waliotoka droo
Bondia Zumba Kukwe kushoto akioneshana umwamba na Josef Njelekela wakati wa mpambano wao waliotoka droo
Kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' kushoto akimpongeza khalid chokolaa baada ya kuibuka mshindi katika mpambano wake
Bondia Tasha Mjuaji kushoto akipambana na Rajabu Mahoja wakati wa mpambano wao

Bondia Mada Maugo kushoto akiwa anapigana na Thomas Mahali mwenye rasta
Bondia Mada Maugo akiwa anazipanga kavukavu na bondia Thomas Mashali walipiokutana katika ukumbi wa Frends Corner Manzese
Na Mwandishi Wetu

MPAMBANO wa ubingwa wa UBO umekosa kutangazwa mshindi mbele ya mashabiki baada ya vurugu kubwa kutokea katika ukumbi wa Friends Corner Manzese Dar es salaam jana.

uUingwa huo uliokuwa ukigombaniwa na mabondia Said Mbelwa na Karama Nyilawila alishindikana kupatikana mshindi baada ya raundi ya nane bondia Karama kumpiga kichwa Mbelwa cha wazawazi na kusababisha Mbelwa kuhamaki kwa kulipiza kisasi na kumsukuma nje pia kumrukia wakati alipotoka nje ya ulingoni mpambano huo wa raundi kumi ulijikuta ukishia kwa raundi nane
Waamuzi pamoja na majaji walikimbia ukumbini wakiwaacha mashabiki bila kuleta majibu ya mpambano huo hata hivyo Mbelwa alirudi ulingoni kwa ajili ya kuendelea kupambana na mpinzani waka alikimbia moja kwa moja kutokana na kuona ngumi za mtaani  ndizo zinashika kasi.
wakati huohuo bondia Mada Maugo alimpiga mwenzake Thomas Mashali kwa ngumi tatu mfululizo
bila kufata sheria ambapo ni kinyume na taratibu za mchezo wa masumbwi duniani. Mabondia hao wote walionekana wamelewa walishindwa kuelewana mbele ya promota Ally Mwazoa
Katika mapambano ya utangulizi yaliyochezwa bondia Khalid Chokoraa ambaye ni mwanamuziki alimpiga kwa KO ya raundi ya kwanza  Abdul Manyenza na Mwaite Juma alimpiga Athumani Rashid wa Tanga kwa pointi wakati Selemani Galile alipigwa kwa pointi na Abdalah Pazi

No comments:

Post a Comment