Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Wednesday, May 21, 2014

Hatimaye Lionel Messi amzidi Ronaldo kwa mshahara, aongeza mkataba Catalunya

Sura zenye furaha: Lionel Messi akisaini mkataba mpya mbele ya Rais wa Barcelona Josep Maria Bartomeu
Lionel Messi ameweka saini ya kuongezea mkatana wake na klabu yake ya Barcelona mkataba ambao utamfanya kuwa mchezaji anayelipwa pesa nyingi zaidi dunia ambapo atakuwa akipokea pauni milioni £16.3 kwa mwaka. 
Mshambuliaji huyo wa Barcelona ameonekana akiwa katika picha na Rais wa klabu hiyo  Josep Maria Bartomeu akisaini mktaba wake mpya ikiwa ni siku mbili baada ya msimu wa ligi kuu ya nchini Hispania La Liga kumalizika.
Messi sasa anakuwa ni zaidi ya nyota wa Real Madrid Cristiano Ronaldo anayelipwa (£15m) kwa mwaka.
He's staying: Lionel Messi has agreed to sign a new deal keeping him at Barcelona
Lionel Messi amekubali mkataba mpya
Boost: Messi agreeing a new deal is the news the Barcelona fans had been waiting for
  Wayne Rooney,ambaye ni mchezaji anayelipwa pesa nyingi nchini England, kwa mwaka anapokea kiasi cha pauni milini £15.6 kwa mwaka ambayo ni sawa na pauni £300,000 kwa wiki.
 
Mkataba wa awali wa Messi umefanyiwa ukarabati kiasi kwamba posho yake hiyo ukiachana na bonasi utakuwa ukifanyiwa marekebisho kila mwaka wa mkataba mpya.
Hiyo maana yake ni kwamba Messi atakuwa akipokea pauni milini £16.3 msimu ujao lakini endapo kama atashinda ligi ya mabingwa bonasi yake itaongezwa na hivyo jumla yake itakuwa ni malipo mapya kuelekea msimu utakao fuata.
Kiwango cha pesa cha uvunjaji wa mkataba cha pauni milioni £250 kimesalia hivy, na hiyo inaweka milango wazi kwa vilabu vyenye njaa ya kupata huduma ya Messi kama vile  Manchester City au Paris Saint-Germain kuweka fedha mezani endapo watafikia kiwango hicho ingawa vita ya mpango wa matumizi mabaya ya fedha FFA( Financial Fair Play ) ikionekana kuwa tishio.
Taarifa ya Catalans iliyotolewa Ijumaa iliyopita imesomeka 
'FC Barcelona imefikia makubaliano ya kufanyia mabadiliko vifungu vya mkataba wa Leo Messi ndani ya klabu, mabadiliko hayo na zoezi la kusainiwa mkataba litafanyika siku chache zijazo'

No comments:

Post a Comment