Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, February 22, 2014

WAYNE ROONEY ASAINI MKATABA MPYA, KUBAKI OLD TRAFFORD HADI JUNI 2019

Wayne Rooney Jana alisaini Mkataba wa mpya wa Miaka minne ambao utamweka Manchester United hadi Juni 2019 na pia kumfanya awe Balozi wa Klabu akistaafu kucheza Soka.
Rooney, mwenye Miaka 28, alisainiwa kutoka Everton Agosti 2004 na amecheza Gemu 430 kwa Man United na kufunga Bao 208 ambayo ni Rekodi iliyomweka awe mmoja wa Wafungaji Bora wa Klabu akikamata Nafasi ya 4 nyuma ya Jack Rowley (Bao 211), Denis Law (237) na Bobby Charlton (249).

Mara baada ya kusaini Mkataba huo, David Moyes aliongea: “Wayne amekuwa ndie Mchezaji Bora wa England tangu nimwingize Timu ya Kwanza ya Everton Mwaka 2003. Tangu niwe Meneja hapa Julai Mwaka Jana nimesikia raha kufanya nae kazi. Nilisema Rooney ana nafasi kubwa kuwa Lejendari wa Klabu na anaweza kuivunja Rekodi ya Sir Bobby Charlton na kuwa Mchezaji wa Kwanza kufikia Bao 250 kwa Klabu hii!”
Nae Wayne Rooney alitamka: “Nimetengenezwa kubaki United! Ikifika Agosti nitakuwa Klabu hii Miaka 10 na nimecheza na Wachezaji mahiri na kutwaa Mataji mengi. Sasa nina nafasi kuendeleza Vijana wengine Klabuni hapa. Mashabiki wamekuwa wazuri sana kwa sapoti yao kubwa kwangu tangu Siku ile nilipoanza na Fenerbahce na kunipa sapoti kubwa!”

Wayne Rooney na Phil Neville kwenye mazoezi kipindi cha nyumaMwaka 2004 Rooney alijiunga na United kutokea EvertonMwaka mmoja baadae 2005 Rooney akatwaa la mwezi
Tena 20052006

20072007 akapewa namba yake ya kudumu
200820092009 hapo hapo akishangilia bao lake la 100 2009 pia akapewa ukapten wa England kwa mara kwanza
2010 alifunga bao nne kwenye mechi moja dhidi ya Hull2010 aliongeza mkataba2011 alifunga bao la heshima na la kiwango dhidi ya City2013 alifunga bao lake la 1502014Rooney na Steven Gerrard kwenye moja ya patashika!!

No comments:

Post a Comment