Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, February 22, 2014

PENATI ALIYOKOSA MESUT OZIL BADO INAMKOSESHA RAHA, WENGER ADAI WAMPE MUDA WA KUSAHAU


Mesut Ozil MENEJA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amesema kiungo wake Mesut Ozil bado anatafunwa na dhambi ya kukosa penati katika mchezo dhidi ya Bayern Munich. Kiungo aliyevunja rekodi katika usajili wake alipata penati ya mapema katika mchezo huo wa Ligi ya Mabingwa barani Ulaya lakini alikosa kwa kumpigia moja kwa moja kipa wa Bayern Manuel Neuer. Akihojiwa Wenger amesema kwasasa wanamuacha asahau yaliyotokea kwasababu yamepita masaa 48 toka akose penati hivyo ni muda mfupi sana. Wenger amesema ana mifano ya wachezaji waliopitia wakati kama wa Ozil akiwemo Dennis Bergkamp ambaye alikosa penati dhidi ya Manchester United mwaka 1999 katika nusu fainali ya Kombe la FA na hakutaka kupiga penati baada ya hapo lakini leo ana sanamu lake nje ya uwanja wao.Kocha wa Arsenal, Arsene WengerOzil juzi alikosa penati!Mesut Ozil akiachia shuti njaa na kudakwa na kipa Never juzi usiku

No comments:

Post a Comment