Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Friday, February 28, 2014

TWIGA STARS YAAGA RASMI MASHINDANO YA AFRIKA BAADA KUTOKA SARE YA 1-1 NYUMBANI









TIMU ya Taifa ya Wanawake(Twiga Stars) imetolewa katika mashindano ya raundi ya kwanza kuwania kufuzu fainali za Mataifa Afrika kwa wanawake baada ya kutoka sare ya bao 1-1 dhidi ya Shepolopolo ya Zambia katika mchezo uliochezwa kwenye Uwanja wa Azam Complex Chamazi, Dar es Salaam. 

Katika mechi ya kwanza iliyochezwa nchini Zambia Twiga Stars ilifungwa mchezo huo kwa mabao 2-1 hivyo imetolewa kwa jumla ya mabao  3-2.

Katika mechi hiyo iliyokuwa na ushindani mkali, Twiga Stars ndio walioanza kupata bao  la  kuongoza dakika ya 39 kupitia kwa Asha Rashid akiwa ameunganishiwa pasi  kutoka kwa Vumilia Maarifa.
Ushindi huo uliipeka Twiga Stars hadi mapumziko ya kipindi cha kwanza bila kuwapa nafasi Shepolopolo waliokuwa wakijitahidi kwa kila namna ili kusawazisha.

Baada ya mapumziko timu zote zilikuwa na ushindani mkali lakini dakika ya 65 Kocha Rogasian Kaijage alifanya mabadiliko katika kikosi chake cha Twiga Stars kwa kumtoa Shelder Boniface na kumwingiza Fatuma Mustafa lakini bado  haikusaidia.

Mnamo dakika ya 80 Shepolopolo walifanikiwa kusawazisha bao la kwanza kupitia kwa Suzan Banda baada ya mchezaji wa Twiga Stars Evelyn Sekikubo kumfanyia madhambi  Mzambia Hellen Mubanga katika eneo la hatari.

Bao hilo lilipigwa moja kwa moja na kuingia golini, baada ya Kipa Fatuma Omar konekana kukaa nyuma ya mabeki waliokuwa wamemziba bila kuona mpira uliokuwa ukigongwa.
Aidha, dakika ya 86 Kocha Kaijage alifanya tena mabadiliko kwa kumtoa Amina Ally na kumwingiza Zena Khamis ili kuleta matunda, lakini ushindani ulikuwa mkali kila upande.

Pamoja na hayo yote, Twiga Stars ilipoteza nafasi nyingi za kufunga ambapo dakika ya 5, 7, 13, 20 walikuwa wakipiga mipira ikipaa na kutoka nje.
Kutokana na kupoteza mchezo huo, Twiga Stars watapumzika hadi mwakani katika michuano mingine.


No comments:

Post a Comment