Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, October 12, 2013

NETHERLANDS 8 v HUNGARY 1, ROBIN VAN PERSIE AWATULIZA HUNGARY KWA HAT-TRICK USIKU HUU ATUPIA BAO TATU PEKE YAKE NA KUVUNJA REKODI YA PATRICK KLUIVERT!, WAKIUA 8-1!

Mchezaji matata Robin Van Persie anayekipiga kwenye Klabu ya manchester United ameifungia Nchi yake bao tatu peke yake kwenye Fainali za Kombe la Dunia Mwakani 2014.
Netherands wameanza kufunga bao dakika ya 16 bao la Robin Van Persie, Dakika ya 25 Mchezaji Kevin Strootman akafunga bao la pili huku bao la tatu likifungwa na Jeremain Lens dakika ya 38. Bao la dakika ya 44 la Robin Van Persie likahitimisha kipindi cha kwanza na kwenda mapumziko zikiwa bao 4-0 dhidi ya Hungary. Bao la pekee la Hungary limefungwa kwa Mkwaju wa penati dakika ya 47 kipindi cha pili. Huku wao Netherlands dakika ya 53 Robin van Persie akiwaongeza bao jingine la tano. Hungary wakijifunga wenyewe kupitia kwa Szilárd Devecseri dakia ya 65. Dakika ya 86 Rafael Van der Vaart akawapatia bao jingine na kufikisha bao 7-1.
Dakika ya 90 mchezaji Arjen Robben akawashona bao la mwisho na la dakika za lala salama na kuifikishia bao 8-1 na mpira kuishia hapo.

Chezea mimi...!! Van Persie kulia akiua ua kiana timu ya Hungary usiku huu na kujiwekea historia ya pekee.
Van Persie akishangilia..

Mpaka ndani!!

Akijiakikishia bao likiingia nyavuni usiku huu

Van Persie akifunga moja ya bao lake kwa kichwa 

Wachezaji wa Uholanzi wakishangilia 

Jeremain Lens akiifungia Uholanzi bao la tatu

Hakunaga: 8-1!!! Wachezaji wa Uholanzi wakipongezana

No comments:

Post a Comment