Mjini
Magharibi imepata tiketi ya kucheza fainali ya michuano ya Copa
Coca-Cola kwa vijana wenye umri chini ya miaka 15 upande wa wavulana
baada ya kuing’oa Temeke kwenye nusu fainali iliyochezwa leo (Septemba
13 mwaka huu) asubuhi Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, jijini Dar es
Salaam.
Ushindi
wa mabao 2-0 yaliyofungwa dakika za 30 na 63 kupitia Juma Ali Yusuf
ndiyo yaliyoipa Mjini Magharibi tiketi ya kucheza fainali itakayofanyika
kesho (Septemba 14 mwaka huu) Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume kuanzia
saa 9 alasiri.
Mjini
Magharibi itacheza fainali hiyo na mshindi wa nusu fainali ya pili
inachezwa leo jioni kwenye uwanja huo huo kati ya mabingwa watetezi
Morogoro na Ilala.
Kwa
upande wa wasichana Ilala imetinga fainali baada ya kuifunga Kinondoni
mabao 2-0 katika nusu fainali ya kwanza. Mabao ya washindi yalifungwa
dakika ya 27 na Fatuma Bahau wakati Happiness Lazoni alifunga la pili
dakika ya 39.
Nusu fainali ya pili kwa wasichana itakuwa kati ya Mwanza na Mbeya.
No comments:
Post a Comment