Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Friday, August 9, 2013

TEVEZ ATUNDIKA DALUGA ARGENTINA, ANCELOTTE:KIPA NAMBA MOJA BADO NA ZAHA ANUKIA KUITWA ENGLAND

Milan, Italia
MSHAMBULIAJI wa Juventus, Carlos Tevez, ametangaza kustaafu rasmi soka la kimataifa.

Nyota huyo raia wa Argentina aliyetua Juventus majira haya ya joto akitokea Man City, alisema: "Imefika mwisho.

“Sina la kuongeza zaidi, nimesema kile ambacho ninajisikia kukieleza, na huo ndiyo mwisho wa shughuli hiyo. Kama nitasema lingine zaidi ya hilo, nitaonekana kama ninaomba kuitwa tena. Upande wa Kimataifa ulikuwa wakati uliopita.”
 
Ancelotti: Kipa namba moja Real bado
Madrid: KOCHA wa Real Madrid, Carlo Ancelotti, amesema bado hajafanya uamuzi wa kipa atakayekuwa chaguo lake la kwanza katika kikosi chake.

Licha ya Ancelotti kumchezesha Iker Casillas  katika ushindi wa mabao 3-1 Real iliyoupata dhidi ya Chelsea juzi, alisema: "Kipindi cha pili, Casillas aliokoa michomo mingi, lakini bado sijachagua kipa namba moja kwa sababu Jumamosi nitamchezesha Diego López na baada ya hapo nitaamua."
 
Zaha anukia kuitwa England
London: WINGA wa Manchester United, Wilfried Zaha, jana alikuwa akitarajiwa kuitwa katika Kikosi cha Wakubwa cha England.

Gazeti la The Daily Mail, lilieleza kuwa kiwango anachokionesha Zaha katika mechi za kujiandaa na msimu mpya kilitarajiwa kumshawishi Roy Hodgson kumuita kwa ajili ya kujiandaa na mechi dhidi ya Scotland Jumanne.


Barca yatolewa 'nduki' kwa Luiz
London: Chelsea imeitoa 'nduki' Barcelona, baada ya kuiambia kuwa haipo tayari kupokea ofa yao ya pauni milioni 34.5 (Sh. bilioni 83.8 za Tanzania) kwa ajili ya kumuuza David Luiz, huku ikiiambia kuwa kamwe isirudi tena kwa kuwa beki huyo wa kati hauzwi.

Sportsmail limeeleza kuwa, Luiz alikuwa chaguo la kwanza katika usajili wa beki wa kati kwa miamba hiyo ya Catalan, lakini Jose Mourinho na uongozi wa Stamford Bridge  umeiambia Barca wala isihangaike kuongeza ofa yao kwa kuwa Mbrazil huyo hauzwi kwa bei yoyote ile.

No comments:

Post a Comment