GHANA, Nchi pekee ya Afrika kutwaa Kombe la Dunia U-20 Mwaka 2009, Jana Usiku huko Turkey, iliwabwaga Chile Bao 4-3 baada Dakika 120 za Robo Fainali ya ya Mashindano ya FIFA ya Kombe la Dunia kwa Vijana chini ya Miaka 20, U-20.
Hadi Dakika 90
kumalizika matokeo yalikuwa Ghana 2 Chile 2.
Ghana walipata Bao la kwanza katika Dakika ya 11 baada ya Frank Acheampong kumtengenezea Moses Odjer alieweka kifuani na kuachia shuti kali lakini Chile walijibu kwa Bao 2 za haraka za Nicolas Castillo na Mchezaji wa Manchester United Angelo Henriquez kwenye Dakika za 23 na 27.
Ghana walifanya Gemu kuwa 2-2 katika Dakika ya 72 kwa Bao la Ebenezer Assifuah na Mechi kuingia Dakika za Nyongeza 30.
Katika Dakika ya 98, Angelo Henriquez aliipeleka Chile kuwa 3-2 lakini Seidu Salifu akaisawazishia Ghana katika Dakika ya 113 na Assifuah kuipa ushindi kwa Bao la 4 katika Dakika ya 120.
Fainali ni Jumamosi Julai 13.
Ghana walipata Bao la kwanza katika Dakika ya 11 baada ya Frank Acheampong kumtengenezea Moses Odjer alieweka kifuani na kuachia shuti kali lakini Chile walijibu kwa Bao 2 za haraka za Nicolas Castillo na Mchezaji wa Manchester United Angelo Henriquez kwenye Dakika za 23 na 27.
Ghana walifanya Gemu kuwa 2-2 katika Dakika ya 72 kwa Bao la Ebenezer Assifuah na Mechi kuingia Dakika za Nyongeza 30.
Katika Dakika ya 98, Angelo Henriquez aliipeleka Chile kuwa 3-2 lakini Seidu Salifu akaisawazishia Ghana katika Dakika ya 113 na Assifuah kuipa ushindi kwa Bao la 4 katika Dakika ya 120.
MAGOLI:
Ghana
4
-Dakika ya 21
Odjer
-72 & 120
Assifuah
-113
Salifu
Chile
3
- Dakika ya 23
Nicolas Castillo
-27 & 98
Angelo Henriquez
Katika Robo Fainali
iliyotangulia Jana Usiku, Iraq mara 3 waliongoza lakini mara zote South Korea
walisawazisha kwenye Mechi ambayo ilimalizika Bao 2-2 katika Dakika 90 na
kuongezwa Dakika za Nyongeza 30.
Katika Dakika hizo
za Nyongeza, Iraq walifunga Bao lao la 3 katika Dakika ya 118 lakini katika
Dakika ya mwisho ya muda wa majeruhi, South Korea walisawazisha katika Dakika ya
122 na ndipo ikaja Tombola ya Mikwaju ya Penati ambazo Iraq walishinda kwa
Penati 5-4 wakati South Korea walipokosa Penati 2 na Iraq 1.
MAGOLI:
Iraq
3
-Dakika ya 21
Atiyah Ali Faez
-42 & 118
Farhan
South Korea
3
- Dakika ya 25 Kwon
Chang Hoon
-50 Lee
Joo-Young
-122
Jung
Nusu Fainali
zitachezwa hapo Jumatano Julai 10 kwa France kucheza na Ghana kisha kufuatia
Iraq v Uruguay.
RATIBA/MATOKEO:
ROBO FAINALI
45 06/07
France 4 Uzbekistan 0
46 06/07
Uruguay 1 Spain 0
47 07/07
Iraq 3 South Korea 3 [Dak 120 3-3, Iraq Washindi Penati
5-4]
48 07/07
Ghana 2 Chile 2 [Dakika 120, Ghana 4 Chile 3]
NUSU FAINALI
49 10/07 18:00
Bursa France v Ghana
50 10/07 21:00
Trabzon Iraq v Uruguay
MSHINDI WA TATU
51 13/07 18:00
Istanbul L49 v L50
No comments:
Post a Comment