Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Sunday, June 30, 2013

TOTTENHAM YAINGIA VITANI NA LIVERPOOL YA KUMNASA MKHITARYAN


Battle: Both Tottenham and Liverpool want to sign Henrikh Mkhitaryan (left) from Shakhtar Donetsk
Ni vita baina ya Tottenham na Liverpool wakimtaka Henrikh Mkhitaryan (kushoto pichani) akitokea Shakhtar Donetsk.
Tottenham imeingia vitani kumnasa Mkhitaryan wakati Liverpool wakiongoza vita hiyo kwa ada ya mezani ya pauni milioni £20.Tottenham inajipanga kutia sumu mpnago wa Liverpool wa pauni £20 kumchukua nyota wa Shakhtar Donetsk kiungo mchezeshaji Henrikh Mkhitaryan.

Bosi wa Anfield Brendan Rodgers ameonekana kuwa kinara wa kukamilisha usajili wa mchezji huyo ambaye anaonekana kuwa ni mwenye kipaji ilhali Spurs kwasasa nao wanaonekana kuwa mbionioni kumnasa nyota huyo wa kimataifa wa Armenia.

Imefahamika kuwa mshauri wa Mkhitaryan amekuwa katika mazungumzo na wakuu wa Tottenham juu ya kusaka uwezekano wa kumpeleka White Hart Lane msimu ujao.
Spurs kwasasa pia wako katika mpango wa kumkamata Puulinho wa Corinthians kwa ada ya uhamisho wa pauni milioni £17 ambaye anatazamiwa kukamilisha mipango ya kuanguka saini baada ya fainali ya michuano ya kombe  la mabara hapo kesho Jumapili. In demand: Champions League finalists Borussia Dortmund have made an offer for Mkhitaryan
Taarifa nyingine zinasema washindi wa pili wa ligi ya mabingwa Ulaya Borussia Dortmund nao wameweka mezani pauni milioni £19.5 kwa ajili ya kiungo huyo mwenye umri wa miaka 24.
Lakini Shakthar wamesisitiza kuwa wanahitajia angalau pauni milioni £25 kwa ajili ya mchezaji huyo ambaye anatakiwa na vilabu vya England kama vile Chelsea na Manchester City.
Spurs wanasalia na matumaini mengine ya kumchukua David Villa pamoja na mshambuliaji mwingine wa Galatasaray Burak Yilmaz mwenye umri wa miaka 27.

No comments:

Post a Comment