

Hii imekuwa mara ya kwanza kwa Cardiff kurejea kwenye ligi ya juu zaidi nchini Uingereza baada ya miaka 51 ya kupambana kwenye ligi ndogo toka waliposhuka daraja mwaka 1962.
Cardiff inakuwa timu ya pili kutoka nchi ya Wales ambayo ni sehemu ya Taifa la Uingereza kushiriki ligi kuu baada ya Swansea iliyopanda daraja misimu miwili iliyopita. Pia inakuwa timu ya 46 tofauti kushiriki ligi kuu nchini England toka ilipoitwa ligi kuu ya England mwaka 1992.



Timu nyingine zitakazopanda daraja msimu ujao kwenye ligi ya Uingereza na zile zitakazoshuka kutoka ligi kuu kwenda ligi ya chini zitajulikana mwishoni mwa mwezi ujao.

No comments:
Post a Comment