Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, January 21, 2013

ZAMBIA VIBONDE WA TAIFA STAR WABANWA MBAVU NA ETHIOPIA WABABE WA STARS LEO



Vibonde wa Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars (Zambia) ambao ni Mabingwa wa Soka bara la Afrika leo wamelazimishwa sare na Wababe wa Stars Ethiopia kwa kufungana 1-1 katika mchezo wao wa kwanza wa kuwania ubingwa wa Afrika
Katika mchezo huo ambao Ethiopia walicheza wakiwa 10 uwanjani, walifanikiwa kufunga bao la kusawazisha katika kipindi cha pili.
Ethiopia ambayo inashiriki michuano hiyo kwa mara ya pili baada ya kipindi cha miaka 30 kupita ilikuwa waandike goli katika dakika 20 za awali baada ya Saladin Seid kupiga mkwaju wa penati uliopanguliwa na mlinda mlango Kennedy Mweene.
Alikuwa ni Collins Mbesuma aliyewanyanyua mashabiki wa Zambia uwanjani hapo na popote pale duniani baada ya kuifungia timu yake goli katika dakika ya 44 kipindi cha kwanza na baadae Adane Girma aliisawazishia Ethiopia katika kipindi cha pili.

Taifa Stars ilichezo michezo miwili ya kirafiki dhidi ya Zambia hapa nyumbani na kushinda 1-0 na baade kucheza na Ethiopia mjini Adis Ababa na kuchapwa goli 2-1.

Michuano ya Mwaka huu ya AFCON imetawaliwa na sare ya bila kufungana au ya kufungana 2-2 au 1-1 huku Mali pekee wakiibuka na ushindi hafifu wa goli 1-0 dhidi ya Niger jana.

No comments:

Post a Comment