Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Friday, August 7, 2015

TWIGA YAENDA KUWEKA KAMBI ZANZIBAR KWA SIKU KUMI




TIMU ya taifa ya Wanawake, ‘Twiga Stars’ imeondoka leo kwenda visiwani Zanzibar kwa ajili ya kambi ya kujiandaa na fainali za Matifa ya Afrika “All African Games’ zinatarajiwa kufanyika nchini Congo Brazaville Septemba mwaka huu.
Akiongea kabla ya kuondoka, Kocha Mkuu, Rogasian Kaijage alisema anashukuru kwani wachezaji wake wanabadilisha mazingira jambo ambalo linaweza kuleta matokeo mazuri kwake japo mazoezi ni yale yale.
“Nimefurahi wachezaji kuondoka kwenye mazingira ya hapa kwani yana mwingiliano wa watu sana kiasi kamba wachezaji hawapumziki ipasavyo kwani mara kaja huyu kuzungumza nao hivyo kuwa mbali italeta utulivu kiasi Fulani”, alisema Kaijage.
Twiga Stars ambayo imefuzu kwa Fainali za Michezo ya Afrika itakayoanza kutimua vumbi Septemba 04 – 17 imepangwa kundi A na wenyeji Congo Brazaville na Nigeria pamoja na Ivory Coast.
Wakati huo huo, katika kujiweka sawa baada ya kukosa michezo ya kimataifa ya kirafiki, Twiga ilicheza na timu ya Ilala Academy ya U-17 na kufungwa mabao 3-0 kwenye Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam.
Mchezo huo ambao ulivuta mashabiki wengi ambao walikuwa wanasubiri kuona mazoezi ya Yanga, uliwavutia mashabiki na kuwafanya kuwashangilia kwani walikuwa wakicheza kwa akili sana kuliko kutumia nguvu.
Mabao ya Ilala Academy yalifungwa na Rajabu Ally ambaye alifunga mabao mawili na msumari wa mwisho ulipigiliwa na Hamza Rajab.


No comments:

Post a Comment