CHEKI KIPIGO CHA HISTORIA CHA BRAZIL TOKA KWA WAJERUMANI
Dakika ya 69 Andre Schürrle aliyeingia
kipindi cha pili nae alijipatia bao kwa kufunga bao la sita na kufanya
6-0 dhidi ya wenyeji Brazil baada ya kupata pasi kutoka kwa Philipp
Lahm.
Dakika ya 79 Andre Schürrle alifunga tena bao la pili na kufanya 7-0 dhidi ya Wenyeji Brazil baada ya kupata mpira kutoka kwa Thomas Müller. Bao la kufutia machozi lilifungwa na Oscar katika dakika ya 90 na Mwamuzi Marco Rodriguez kutoka
Mexico alipuliza kipenga na kumaliza mpira huo ambao Germany
walijipatia ushindi mnono wa Bao 7-1 kwenda Fainali. Ushindi huo
unawafanya wasubiri mshindi wa kesho kati ya Argentina na Netherlands.
Sherehe kwa Germany!!!!
Kipa Never akiokoa shuti langoni mwake
Marcelo akificha uso wake ndani ya Nyavu
Khedira nae alichana nyavu
Taswira!!
Tumevurugwa!!!
Beki wa Brazil David Luiz kulia akiwa hoi!!! kajiinamia akijiuliza!!! kuna nini leo!
Mapumziko 5-0
WENYEJI Brazil Usiku huu wamepewa kipigo kikubwa katika Historia ya Kombe la Dunia baada Germany kuwabamiza Bao 7-1 katika Mechi ya Nusu Fainali na kutinga Fainali.
Dakika ya 23 Miroslav Klose, Dakika ya 24 Toni Kroos, Dakika ya 26 tena Toni Kroos akafunga bao la nne na dakika ya 29 Sami Khedira akaifungia bao la tano na kufanya 5-0 dhidi ya wenyeji Brazil akipewa pasi na Mesut Özil anayekipiga katika Ligi kuu ya England katika klabu ya Arsenal.
Klose akishangilia ba lake
Bao
hizo tano zilihitimishwa na kumaliza kipindi cha kwanza wenyeji Brazil
wakiwa hoi! Wakiwa nyuma ya bao 5-0 kichapo kikubwa katika Hili Kombe la
Dunia mwaka huu 2014 kwa Wenyeji.
Brazil hoi!!!
Toni kroos nae alipachika bao
Kocha wa Brazi Fellipe hana hamu!!! CV hana tena!!
Miroslav Klose
Balaa leo!!! Tutajificha wapi??
4-0!!!!
Klose anavunja Historia na kuweka Historia mpya!!!
Kipindi
cha kwanza dakika ya 11 Thomas Müller aliipachikia bao la kwanza
Germany nakufanya 1-0 dhidi ya Wenyeji Brazil baada ya kupigwa kona na
Toni Kroos.
Thomas Muller alianza kwa kuwafungulia bao hapa Germany
Wachezaji wa Germany wakipongezana
Mashabiki
Kikosi cha Brazil kilichoanza
Kikosi cha Germany
Wimbo wa Taifa wa Wenyeji Brazil uliimbwa
Kipa wa Germany Manuel Never alianza kwa kudaka shiti kwa kile Brazil walianza mtanange kwa kasi sana
Mashabiki wa Brazil tayari kwa kushangilia timu yao.
VIKOSI:
Brazil: Julio Cesar, Maicon, Dante, Luiz, Marcelo, Gustavo, Fernandinho, Hulk, Oscar, Bernard, Fred.
Subs: Jefferson, Dani Alves, Paulinho, Maxwell, Henrique, Ramires, Hernanes, Willian, Jo, Victor.
Germany: Neuer, Lahm, Boateng, Hummels, Howedes, Schweinsteiger, Khedira, Muller, Kroos, Ozil, Klose.
Subs: Zieler, Grosskreutz, Ginter, Schurrle, Podolski, Draxler, Durm, Mertesacker, Gotze, Kramer, Weidenfeller.
Referee: Marco Rodriguez (Mexico)
WENYEJI Brazil Usiku huu wamepewa kipigo kikubwa katika Historia ya Kombe la Dunia baada Germany kuwabamiza Bao 7-1 katika Mechi ya Nusu Fainali na kutinga Fainali.
Dakika ya 23 Miroslav Klose, Dakika ya 24 Toni Kroos, Dakika ya 26 tena Toni Kroos akafunga bao la nne na dakika ya 29 Sami Khedira akaifungia bao la tano na kufanya 5-0 dhidi ya wenyeji Brazil akipewa pasi na Mesut Özil anayekipiga katika Ligi kuu ya England katika klabu ya Arsenal.
VIKOSI:
Brazil: Julio Cesar, Maicon, Dante, Luiz, Marcelo, Gustavo, Fernandinho, Hulk, Oscar, Bernard, Fred.
Subs: Jefferson, Dani Alves, Paulinho, Maxwell, Henrique, Ramires, Hernanes, Willian, Jo, Victor.
Germany: Neuer, Lahm, Boateng, Hummels, Howedes, Schweinsteiger, Khedira, Muller, Kroos, Ozil, Klose.
Subs: Zieler, Grosskreutz, Ginter, Schurrle, Podolski, Draxler, Durm, Mertesacker, Gotze, Kramer, Weidenfeller.
Referee: Marco Rodriguez (Mexico)
You might also like:
Post a Comment